HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 16, 2018

SERIKALI YAMCHARUKIA MKANDARASI DOTT

  Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akitoa maelekezo kwa Mkandarasi Dott Service na Mhandisi Mshauri kutoka Kampuni ya Kyongdong Engineering wanaojenga barabara ya Mtwara – Mnivata yenye urefu wa KM 50 kwa kiwango cha lami na kumtaka Mkandarasi huyo kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo haraka.   Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya  Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
  Mbunge wa Jimbo la Nanyamba mkoani Mtwara, Mheshimiwa Abdallah Chikota (Wa kwanza kulia), akimuonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, (Wa pili kulia) sehemu yenye mteremko mkali katika mlima wa Nameleche uliopo katika barabara ya Mtwara-Mnivata-Tandahimba-Newala hadi Masasi yenye urefu wa KM 210 ambapo magari husumbuka katika kipindi cha mvua kutokana na mteremko huo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mnivata mkoani Mtwara alipofika hapo kukagua barabara ya Mtwara – Mnivata yenye urefu wa KM 50 inayojengwa kwa kiwango cha lami.

No comments:

Post a Comment

Pages