HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 08, 2018

Tatu Mzuka yazidi kuwaneemesha Watanzania,wengi waendelea kujizolea mamilioni


Mwakilishi wa Kampuni ya inayochezesha mchezo wa kubahatisha,TatuMzuka,Kemilembe Mbeikya (katikati),akizungumza mbele ya Wanahabari mapema jana wakati wa kuwatambulisha washindi wa TatuMzuka,ambao kulia ni Abraham Kisiri kutoka Mkwajuni Kinondoni aliyejishindia million 60 pamoja na Ummy Abraham kutoka Wazo hill, Tegeta alijishindia million 5.



Kemi alisema kuwa Tatu Mzuka jackpot ya wiki iliyopita imetoa jumla million 80 kwa washindi wa nne,wakiwemo wawili pichani na wengine ni Mathew Mtoni kutoka Songea aliyejishindia milioni 10 pamoja na Selemani Mkoko kutoka Nachingwea aliejishindia millioni 5.

Tatu Mzuka hadi leo imetoa billion 14 na kutengenza washindi million 6. Hawa washindi ni thibisho tosha kuwa Tatu Mzuka inabadilisha maisha ya watu.Kama unavyojua, Tatu Mzuka inakupa nafasi ya kushinda kila lisaa hadi million 6, na sasa hivi kwenye msimu wa Valentine, wewe na mpendanao mnaweza kushinda million kumi kila silku na bado una nafasi ya kushinda million 60 jumapili hii.
Ummy Abraham amabae ni wa Wazo hill, Tegeta jijini Dar Es Salaama akieleza namna alivyojishindia kitita cha shilingi million 5.Amesema kwa sasa fedha hizo zitamsaidia kuendelea kumsadia katika Matibabu ya Mumewe ambaye ni mgonjwa na pia Fedha nyingine amepanga kumaliza ukarabati wa nyumba zake mbili ili ziendelee kumuingizia kipato.Aidha Ummy ameishukuru TatuMzuka kwa kuleta mchezo ambao kwake umekuwa kama mkombozi kwa wakati aliokuwa nao kwa sasa.
Abraham Kisiri kutoka Mkwajuni Kinondoni jijini Dar,ambaye ni Dereva wa taasisi ya UVCCM alijishindia milioni 60.Abraham ameishukuru Tatu Mzuka kwa kuuleta mchezo huo kwa Wananchi,kwani umekuwa na manufaa makubwa kwa baadhi yao kiasi hata ya kuyabadilisha maisha yao,anasema kwa sasa fedha hizo atazitumia kujiimarisha zaidi kiuchumi .
Mwakilishi wa Kampuni ya inayochezesha mchezo wa kubahatisha,TatuMzuka,Kemilembe Mbeikya (katikati),akiwa na Washindi wa washindi wa TatuMzuka,ambao kulia ni Abraham Kisiri kutoka Mkwajuni Kinondoni aliyejishindia million 60 pamoja na Ummy Abraham kutoka Wazo hill, Tegeta alijishindia million 5 wakiwa sambamba na mfano wa hundi zao.

No comments:

Post a Comment

Pages