HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 22, 2018

MKUU WA WILAYA YA MTWARA AKAGUA ENEO LA CHUO CHUO CHA KILIMO MATI MKOANI MTWARA LILILOVAMIWA NA WANANCHI


Mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Mtwara Bw. Evod Mmanda jana machi 21/2018 ametembelea eneo la Chuo cha Kilimo MATI mkoani Mtwara ili kujionea uvamizi uliofanywa na baadhi ya wananchi kwenye eneo la chuo ambapo wavamizi wamefyeka na kupanda mazao ya kudumu kuashiria kujitwalia isivyo halali maeneo hayo.

Mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Mtwara Bw. Evod Mmanda akijadiliana jambo na baadhi ya wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Mtwara wakati walipokagua eneo la chuo cha Mati Mtwara lililovamiwa na wananchi.

Mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Mtwara Bw. Evod Mmanda akimsikiliza Mmoja wa wazee majirani walioshuhudia wakati serikali ikitwaa eneo hilo la hekta 560 na kuwalipa fidia wenyeji mwaka 1974 wakati akiongea na kamati

Mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Mtwara Bw. Evod Mmanda akizungumza baadhi ya wajumbe wakati wa ukaguzi wa eneo hilo la hekta 560 ambalolimevamiwa na wananchi.

Mkuu wa wilaya na Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya Mtwara Bw. Evod Mmanda akizungumza baada ya kukagua eneo hilo la hekta 560 ambalo serikali ililitwaa na kuwalipa fidia wenyeji mwaka 1974.

No comments:

Post a Comment

Pages