HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 05, 2018

NSSF MABINGWA TAMASHA LA PASAKA 2018

TIMU ya soka ya Shirika la Taifa ya Hifadhi ya Jamii (NSSF), imeichapa bila huruma timu ya soka ya ZSSF 2-0 katika mchezo wa tamasha la Pasaka.

Mchezo huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro kwa kuzikutanisha timu mbili za mashirika ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF na ZSSF ambapo lengo la michizo hiyo ni kuimarisha ushirikiano na uhusiano baina ya mashirika hayo mawili.

Mchezo huo uliianza kwa kasi kubwa iliwachukua dakika 4 NSSF kujipatia bao la kwanza baada ya mwamuzi wa mchezo huo Fikiri Yusuph kutoa Penalti baada ya beki wa ZSSF kuunawa mpira katika harakati za kuokoa, mshambuliaji wa NSSF Said Mwinyi aliipiga penalti hiyo na kuipatia timu yake bao la kwanza.


Kuingia kwa bao hilo la mapema kuliwafanya ZSSF kucharuka na katika dakika ya 10 nusura wajipatie bao la kusawazisha baada ya shuti kali lililopigwa na Juma Mbwana kugonga mwamba na kuokolewa na walinzi wa timu ya NSSF.

ZSSF waliendelea kulisakama lango la NSSF lakini walinzi wa timu ya NSSF wamkiongozwa na beki wa wa timu hiyo Hemed Kagobe waliweza kuondoa hatari hizo na kuwapa wakati mgumu washambuliaji wa timu ya ZSSF.

Katika dakika ya 27 ya mchezo nusura ZSSF wapate bao la kusawazisha lakini golikipa wa NSSF, Sadick aliweza kuokoa kiki iliyopigwa na Rashid Suleimani na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.

Time hizo zilirndelea kushambuliana kea zamu hadi mapumziko NSSF ilitoka ikiwa inaongoza 1-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko ambapo ZSSF waliwatoa, Hassani Omar, Abasi Yahaya Abasi, Maulid Suleiman na Hamis Thani na nafsa zao kuchukuliwa na Yusuf Said, Abdulkarim Rajabu, Khamis Haji na Mohamed haji Khamis. 

NSSF waliwatoa Nassoro Nassor, Ally Chuo, mfungaji wa bao la kwanza Said Mwinyi, Sadick Jongo na nafasi zao kuchukuliwa na Bakari Becco, Mwinyi Mzee, Prosper Lyoba na Shaban Enzi.

Mabadiliko hayo yalibadilisha sura ya mchezo katika dakika ya 82 mshambuliaji wa timu ya NSSF, Katunguja aliifungia timu ya bao la pili banda ya kupokea pasi kutoka kwa  Mwinyi Mzee aliyeingia kipindi cha pili, kuingia kwa bao hilo kuliongeza kasi ya mchezo ambapo ZFF walikuja juu wakitaka kupata bao angalau la kufutia machozia lakini kikwazo kikubwa alikuwa mlinda mlango wa timu ya NSSF, Sadick ambaye alikuwa nyota ya mchezo kwa kuokoa mashuti yaliyokuwa yakielekezwa langoni mwake.

Wakati huohuo katika mchezo wa netiboli timu ya NSSF ilingára vilivyo baada ya kuichapa ZSSF kwa jumla ya magoli 23-19 na kunyakua kombe la michuano hiyo kwa mwaka 2018.

Akizungumza wakati akitoa zawadi kwa washindi wa michezo hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa NSSF, Dominick Mbwete, alisema kuwa michezo hii imelenga kujenga ushirikiano baina ya mifuko, kuimarisha uhusiano na pamoja na kuboresha afya kwa wadu wa michezo kupitia mifuko hiyo.

“Lengo la mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka kwa kukutanisha wanamichezo mbalimbali kutoka katika mashirika  ya ZSSF na NSSF ambapo kushiriki kwa pamoja michezo mbalimbali pamoja na kutoa zawadi kwa wanamichezo vote walioshiriki katika tamasha hilo."

ambapo mwakani itafanyika mjini Zanzibar na kuandaliwa na ZSSF watakuwa wenyeji wa michezo hiyo Zanzib imelenga kujenga ushirikiano baina ya mifuko, kuimarisha ushirikiano baina ya ZSSF na NSSF pia imelenga kujenga ushirikiano, uhusiano baina ya wafanyakazi kutoka ZSSF pamoja na NSSF  katika kuimarisha ushirikiano.
Wanamichezo kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) wakipokelewa na wenzao wa NSSF katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kuwasili katika michezo ya tamasha la Pasaka.
Wanamichezo kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) wakipokelewa na wenzao wa NSSF katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kuwasili katika michezo ya tamasha la Pasaka.


 Mapokezi.
Ofisa wa NSSF, Pili Mogella (kulia), akimkaribisha Ofisa wa ZSSF.  
 ZSSF wakiwasili bandarini.
 Wachezaji wa ZSSF wakiwa ndani ya basi.


Kocha wa timu ya netiboli ya NSSF, Joseph Ngánza akitoa maelekezo kwa wachezaji wake. 
 Kocha wa timu ya ZSSF, Hadia Ahmada, akitoa maelekezo kwa wachezaji wake.
Meneja wa Mahusiano na Masoko wa NSSF, Salim Kimaro, akikagua timu ya netiboli ya ZSSF.

Meneja Mahusiano na Masoko wa NSSF, Salim Kimaro akikagua timu ya netiboli ya NSSF.
 Kikosi cha timu ya ZSSF.
Kikosi cha NSSF.
Mshambuliaji wa timu ya netiboli ya ZSSF, Mwasiti Vita, akiwa katika harakati za kufunga huku Amina Jumanne (kushoto), wa NSSF akijaribu kumzuia katika mchezo wa tamasha la Pasaka uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
 Mchezaji wa NSSF, Maliti, akimiliki mpira huku akizongwa na mchezaji wa ZSSF, Yasinta (GD).
 Mchezaji wa timu ya netiboli ya NSSF, Fatuma Sule (C), akichuana na mchezaji wa ZSSF, Fatuma Sule (kushoto).
  Mchezaji wa timu ya netiboli ya NSSF, Fatuma Sule (C), akimiliki mpira.
 Timu ya netiboli ya NSSF wakiwa katika mazoezi.
Meneja wa Mahusiano na Masoko wa NSSF, Salim Kimaro (kulia), akizungumza na wachezaji kabla ya kuanza kwa mchezo wa netiboli ya ZSSF.
 Timu ya NSSF ikiwa mapumziko.
Mashabiki wa timu ya netiboli ya NSSF. 
 Wachezaji wa ZSSF wakiwa katika mazoezi
 Kocha wa timu ya soka ya NSFF, Sanifu Lazaro.
Zawadi za washindi.
Mshambuliaji wa NSSF, Katunguja, akimtoka Rashid Suleiman wa ZSSF (kulia).
Shaban Enzi (kulia), akichuana na Ismail Hubi wa ZSSF.
Ally Chuo wa NSSF (chini), akichuana na Rajabu Said wa ZSSF.
Wachezaji wa NSSF wakishangilia bao la pili la timu hiyo.
Mchezaji wa ZSSF, Seif Hafidh (kulia), akichuana na Said Mwinyi wa NSSF.
 Nahodha wa timu ya netiboli ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Pili Mogella, akipokea kombe la Ubingwa wa michuano ya tamasha la Pasaka kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa NSSF, Dominick Mbwete (kushoto), baada ya kuifunga ZSSF magoli 23-19  katika mchezo ulifanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dominick Mbwete (kushoto), akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya soka ya NSSF, Mzee Mfaume, baada ya kuwafunga ZSSF mabao 2-0 katika mchezo wa tamasha la Pasaka uliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
 Wachezaji wa timu ya soka ya NSSF wakiwa katika picha ya pamoja.
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dominick Mbwete (kushoto), akipokea zawadi ya mlango kutoka kwa Kaimu Meneja wa Rasilimali Watu na Utawala wa ZSSF, Abdallah Mbwana.
Maofisa wa NSSF na wale wa ZSSF wakiwa katika picha ya pamoja katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara ya michezo ya tamasha la Pasaka.
Maofisa wa NSSF na wale wa ZSSF wakiwa katika picha ya pamoja katika bandari ya Dar es Salaam baada ya kumaliza ziara ya michezo ya tamasha la Pasaka.

No comments:

Post a Comment

Pages