HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 13, 2018

AZANIA BANK YAWAFUTURISHA WATEJA WAKE NA WATOTO YATIMA DAR

Na Mwandishi Wetu
AZANIA Benki inajivunia uzalishaji wa huduma kwa kila mmoja kwa wateja wake bila kujali dini, kabila na jinsia kwa faida na hasara kwa kuandaa futari pamoja na waislamu walioungana na wateja wa benki hiyo.
Akizungumza juzi katika hafla ya futari iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara  wa Benki hiyo, Rhimo Nyansaho alisema wameungana na waislam katika futari hiyo ikiwa ni sehemu yao ya kushirikiana na jamii.
Nyansaho alisema benki hiyo inasonga mbele kwa sababu ya michango ya jamii katika benki hiyo ndio maana kipindi cha mfungo wakaona ni sahihi kurudisha pato hilo kwa kufuturu na jamii yenye uhitaji kama watoto yatima na wengineo.
Mkurugenzi huyo alitumia fursa hiyo kuisifia benki yake kwamba wanatoa huduma bora na ndio maana faida inayoongezeka wanairudisha kwa jamii.
Aliipongeza serikali kwa kuweka mazingira ya kushuka kwa riba katika benki mbalimbali ingawa wao walishashusha riba zao muda mrefu.
Mwakilishi wa wateja wa benki hiyo, Deogratius Kifumani aliipongeza benki hiyo kwa huduma zake inazotoa na kutoa wito kwa jamii kuelekeza mikakati yao ya kiuchumi huko.
Kifumani alisema ubora wa huduma zao ndio maana inafanikisha matukio muhimu kama hayo katika jamii kwa kurudisha sehemu ya pato lao.  
Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Maulid Kidebe alisema kilichofanywa na benki ya Azania kina maana kubwa kwa jamii, tukio hilo ni thawabu kubwa zinapatikana kwa sababu imewakumbuka yatima ambao wanatakiwa kuwa karibu zaidi na jamii.
Sheikh Kidebe alitoa wito kwa benki na taasisi nyingine kuiga mfano uliofanywa na Azania ili kusaidia jamii katika mahitaji muhimu.
Mtoto yatima aliyekuwepo katika futari hiyo, Safina Muhsin aliishukuru na kuiomba benki hiyo kuendelea kuwa karibu nao kwa masuala mbalimbali.
Katika hafla hiyo ya futari iliyoandaliwa na benki ya Azania iliwahusisha watoto wa kituo cha Yatima cha Ijango Zaidia cha Sinza jijini Dar es Salaam.
 Watoto wa wanaolelewa katika Kituo cha Yatima cha Ijango Zaidia cha Sinza jijini Dar es Salaam wakiswali kabla ya kujumuika na wateja wa Azania Bank katika futari.
 Sheikh wa Wilaya ya Ubungo, Shjeikh Maulid Kidebe. akiwaongoza wateja wa Azania Bank wakati wa futari iliyoandaliwa na benki hiyo iliyowahusisha watoto wa kituo cha watoto yatima cha Ijango zaidia cha Sinza jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wateja wa Azania Bank wakipata futari iliyoandaliwa na benki hiyo na kuwahusisha watoto wa kituo cha yatima cha Ijango Zaidia cha Sinza jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wateja wa Azania Bank wakipata futari iliyoandaliwa na benki hiyo na kuwahusisha watoto wa kituo cha yatima cha Ijango Zaidia cha Sinza jijini Dar es Salaam.
Watoto wakipata futari.
Wateja wakipata futari.
Watu mbalimbali wakipata futari.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Azania Bank pamoja na wateja wa benki hiyo wakipata futari.
Watoto Yatima wanaolelewa na Kituo cha Ijango Zaidia wakipata futari.
 Baadhi ya Watoto Yatima wanaolelewa na Kituo cha Ijango Zaidia wakipata futari.
Watoto wa kituo cha Yatima cha Ijango Zaidia wakisoma duwa.
Ofisa Masoko Mwandamizi wa Azania Bank, Othman Jibrea, akizunguma katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake pamoja na watoto yatima wa kituo cha Ijango Zaidia cha Sinza.
 Mteja wa Azania Bank, Deogratius Kufumani, akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wateja wa benki hiyo.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara  wa Azania Bank, Rhimo Nyansaho, akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake na kuwahusisha watoto yatima wa kituo cha Ijango Zaidia cha Sinza.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara  wa Azania Bank, Rhimo Nyansaho, akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake na kuwahusisha watoto yatima wa kituo cha Ijango Zaidia cha Sinza.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara  wa Azania Bank, Rhimo Nyansaho, akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake na kuwahusisha watoto yatima wa kituo cha Ijango Zaidia cha Sinza.
 Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Maulid Kidebe, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Azania Bank kwa ajili ya wateja wake pamoja na watoto yatima.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara  wa Azania Bank, Rhimo Nyansaho, akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo.

No comments:

Post a Comment

Pages