HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 25, 2018

LUGALO YATAMBA MASHINDANO YA GOFU YA WAZI

Klabu  ya Lugalo imedhihirisha ubora wao wa mchezo wa gofu hapa nchini  baada ya kushinda mashindano ya TANAPA Lugalo open  yaliyomalizika jumapili jioni kwenye viwanja vya Lugalo.
Mashindano hayo ya Gofu ya TANAPA Lugalo open  yalishirikisha wachezaji zaidi ya 150 kutoka vilabu vya Arusha Gymkhana,Moshi Gymkhana,TPC,Morogoro Gymkhana na Lugalo club.
Ushindi walioupata klabu ya Lugalo katika mashindano hayo  ni wa kujivunia ,kwani katika mashindano yalifanyika mwezi uliopita kwenye viwanja vya Moshi Gymkhana klabu ya Lugalo iliweza kushinda.
Katika mashindano ya TANAPA Lugalo open  ilianza kwa mchezaji wa Taifa Godfrey Gwacha kupata ushindi wa jumla  upande wa Gross.
Mchezaji huyo aliweza kupata ushindi wa jumla baada ya kupiga mikwaju gross  149 ambapo siku ya kwanza mchezaji huyo aliweza kupata gross 76 na siku ya pili akapata gross 73.
Nafasi ya pili ilichukuliwa tena na  Richard Mtweve kutoka Lugalo aliyepiga mikwaju ya gross 152  
Lugalo tena iliweza kutamba upande wa neti baada ya  Agrey John kupata ushindi wa jumla kwa kupiga mikwaju ya neti 138,akifuatiwa   na Anold Simoni kutoka Dsm Gymkhana  aliyepata neti 139.
Kwa upande wa Division A mshindi alikuwa naodha wa klabu ya Lugalo shabani Kibuna aliyeshinda kwa mikwaju ya neti 142 akifuatiwa Isiaka Daud pia  kutoka Lugalo aliyepata neti 143.
Upande wa  Division B mshindi alikuwa Gerald Gadiel kutoka Lugalo aliyeshinda kwa mikwaju ya neti 139 akifuatiwa na Tiger Lee kutoka Lugalo aliyepata neti 147.
Lugalo ilizidi kunyanyasa tena kwenye mashindano hayo  upande wa Division C  baada Magoti Fabiani kushinda kwa upigaji wa  mikwaju ya neti 144 akifuatiwa na Ton H.D  pia wa Lugalo aliyepata neti 145.
Upande wa wanawake nafasi hiyo ilikwenda kwa  Habiba Juma  aliyeshinda kwa mikwaju ya neti  147 akifuatiwa na Khadija Selemani aliyepata neti 149 wote kutoka Lugalo..
Kwa upande wa upigaji mipira kwa karibu nafasi hiyo ilikwenda  kwa Leo Bashiri kutoka Lugalo,na upande wa  upigaji wa mipira ya mbali kwa wanawake nafasi hiyo ilikwenda kwa Neema Olomi kutoka Arusha Gymkhana

No comments:

Post a Comment

Pages