HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 12, 2018

Mawakala Halo Pesa kuweka na kutoa fedha NMB

 Kaimu Mkuu wa wateja wa kati na wadogo wa NMB, Boma Raballa, na Naibu Mkurugenzi wa Halo Pesa, Vu Tuan Long, wakisaini mkataba wa ushirikiano utakaowawezesha mawakala wa Halo Pesa kutumia huduma za Kibenki za NMB kupitia huduma kabambe kwa wakala (Siper-Agent Service) kwa ajili ya kuweka na kutoa fedha kupitia benki hiyo.
Kaimu Mkuu wa wateja wa kati na wadogo wa NMB, Boma Raballa, na Naibu Mkurugenzi wa Halo Pesa, Vu Tuan Long, wakionyesha mkataba wa ushirikiano utakaowawezesha mawakala wa Halo Pesa kutumia huduma za Kibenki za NMB kupitia huduma kabambe kwa wakala (Siper-Agent Service) kwa ajili ya kuweka na kutoa fedha kupitia benki hiyo.
Naibu Mkurugenzi wa Halo Pesa, Vu Tuan Long, akizungumza na waandishi wa habari. 
 Kaimu Mkuu wa wateja wa kati na wadogo wa NMB, Boma Raballa, akizungumza katika hafla ya kusaini mkataba wa ushirikiano wa kibiashara utakaowawezesha mawakala wa Halo Pesa kutumia huduma za Kibenki za NMB kupitia huduma kabambe kwa wakala (Siper-Agent Service) kwa ajili ya kuweka na kutoa fedha kupitia benki hiyo.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Halotel, Mhina Semwenda, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa hafla fupi ya kusaini makubaliano ya kibiashara na benki ya NMB.
 Baadhi ya waandishi wa habari katika hafla hiyo.

Na Costancia Nkindi

KATIKA kutekeleza azma ya kuboresha utoaji huduma za kifedha kwa wananchi wenye vipato tofauti, Kampuni ya mawasiliano ya Halotel na Benki ya NMB  zimeingia katika ushirikiano utakaowawezesha mawakala wa Halo Pesa kutumia huduma za Kibenki za NMB kupitia huduma kabambe kwa wakala (Super-Agent service) kwa ajili ya kuweka na kutoa fedha kupitia benki hiyo.
Hatua hiyo itawawezesha mawakala wote wa huduma za kifedha kupitia Halopesa nchi nzima kuweza  kuweka na kutoa pesa taslim kupitia tawi lolote la benki ya NMB  na kuweza kuwanufaisha mamilioni ya watanzania na huduma za kifedha kwa njia ya mtandao kwa ukaribu na urahisi zaidi.
Naibu Mkurugenzi wa Halo Pesa, Vu Tuan Long amesema ushirikiano huo ni hatua nyingine kubwa katika utoaji wa huduma  za kifedha kupitia mawakala ambapo sasa huduma ya kutoa na kuweka pesa kwa mawakala zitafanyika kupitia benki ya NMB.
“Huduma za kifedha kwa njia ya mtandao ni sekta inayokuwa kwa kasi hapa nchini. Ushirikiano huu utawawezesha mawakala wa Halo Pesa kuweza kupata huduma ya kuweka na kutoa pesa kiurahisi kupitia matawi yote ya NMB  nchi nzima,” alisema Long.
Alisema  hadi sasa hivi Halotel ina mawakala zaidi ya 55,000 walioenea nchi nzima. Mawakala wa Halo Pesa watatumia namba za USSD za Halo Pesa  ambazo ni (*150*88#) kwa kutoa fedha katika benki ya NMB pamoja na kutoa pesa  kwa fomu maalum za kuweka fedha wakiwa katika matawi ya benki hiyo.
Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa wateja wa kati na wadogo wa NMB, Boma Raballa alisema benki hiyo imekuwa ya kwanza katika kutoa huduma zenye ubunifu ambazo zinalenga kutatua changamoto mbalimbali ndani ya jamii, “Tulitambua kuna  uhitaji katika upatikanaji wa fedha kwa mawakala” alisema Raballa.
“Mtandao mkubwa wa matawi yetu unaoenda sambamba na kaulimbiu yetu ya “Karibu nawe” imekuwa sehemu kubwa ya mafanikio katika utoaji  wa huduma za kifedha. Hadi sasa tuna matawi zaidi ya 220 ambayo yako zaidi ya asilimia 98 ya wilaya za nchi hii zitarahisisha sana upatikanaji wa huduma kwa mawakala”. Alisema Raballa.
Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoripotiwa kuwa na watumiaji wengi wa huduma za kifedha wakifikia takribani milioni 19, hivyo uhitaji na upatikanaji wa fedha kwa watumiaji hao imekuwa ni changamoto kubwa kwa baadhi ya watumiaji, kupitia benki ya NMB sasa mawakala na watoa huduma za kifedha sasa watakuwa na nafasi ya kupata huduma karibu yao.

No comments:

Post a Comment

Pages