HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 15, 2018

TATU MZUKA YAZINDUA ‘SUPA MZUKA CUP’ YA MILIONI 300


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Sebastian Maganga, akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari mapema leo jijini Dar,wakati wakizindua ushirikiano na VODACOM, ambapo wateja wa MPESA wataweza kushinda dakika za bure, intaneti na bidhaa mbalimbali kwa kipindi chote cha kampeni pichani kulia ni Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya biashara na Masoko wa MPESA, Bwana Polycarp Ndekana,mbali ya kushirikiana huko.

Tatu Mzuka wamezindua kampeni mpya ya ‘SupaMzuka Cup’ ambapo siku ya fainali tarehe 15 Julai 2018 mshindi mmoja ataondoka na milioni 300 za kitanzania.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Sebastian Maganga Tatu Mzuka pamoja na Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya biashara na Masoko wa MPESA, Bwana Polycarp Ndekana wakionesha kombe wakati wa wakizindua kampeni mpya ya ‘SupaMzuka Cup’ ambapo siku ya fainali tarehe 15 Julai 2018 mshindi mmoja ataondoka na milioni 300 za kitanzania.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Sebastian Maganga Tatu Mzuka pamoja na Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya biashara na Masoko wa MPESA, Bwana Polycarp Ndekana wakionesha jezi maridhawa wakati wa wakizindua kampeni mpya ya ‘SupaMzuka Cup’ ambapo siku ya fainali tarehe 15 Julai 2018 mshindi mmoja ataondoka na milioni 300 za kitanzania.

• Pia yazindua ushirikiano na VODACOM ambapo wateja wa MPESA wataweza kushinda dakika za bure, intaneti na bidhaa mbalimbali kwa kipindi chote cha kampeni.

14th June 2018

Tatu Mzuka, mchezo wa namba unaoongoza nchini Tanzania leo umezindua kampeni mpya ya ‘SupaMzuka Cup’ ambapo siku ya fainali tarehe 15 Julai 2018 mshindi mmoja ataondoka na milioni 300 za kitanzania.

Wachezaji wote wa Tatu Mzuka kuanzia leo mpaka fainali, wataweza kuingia moja kwa moja kwenye droo ya kushinda milioni 300 ambapo kwa kila shilingi 500 unayocheza inakupa tiketi ya kushiriki droo siku ya fainali.

‘Mpaka sasa hii ndiyo kampeni inayosisimua zaidi kwa sababu hakuna ushindi mkubwa namna hii wa jackpot ambao ulishawahi kutolewa nchini Tanzania’ alisema Bwana Sebastian Maganga, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka

Kwa kuwa huu ni msimu wa kucheza na kushinda na marafiki, Tatu Mzuka kupitia droo ya Mzuka Deile wanatotoa fursa kwa mshindi kuchagua marafiki wanne ambapo kila mmoja atapewa 500,000 katika ushindi wa milioni 10 zinazotolewa kila siku.

Katika droo ya Jumapili, marafiki 5 kila mmoja atapata milioni 1 kutoka katika ushindi wa jackpot ya kila Jumapili. Siku ya fainali, mshindi wa milioni 300 atatoa milioni 1 kwa marafiki zake kumi ili kukamilisha timu ya ushindi ya watu 11.

Ili kushiriki kwenye Jackpot ya Supa Mzuka Cup, cheza Tatu Mzuka kupitia; MPESA, TIGO PESA na AIRTEL MONEY, unaingiza namba ya kampuni ambayo ni 555111 na baada ya hapo ingiza namba zako 3 za bahati kisha ingiza kiasi kuanzia shilingi 500 mpaka 30,000.

Akiongea katika tukio la uzinduzi huo Mkuu wa kitengo cha Maendeleo ya biashara na Masoko wa MPESA, Bwana Polycarp Ndekana alisema kwamba kampeni ya SupaMzuka Cup itawanufaisha watumiaji wa Mpesa kipindi chote cha fainali za kombe la dunia, ambapo watashinda sio tu muda wa maongezi na intaneti bali pia zawadi mbalimbali na fedha mpaka siku ya fainali tarehe 15 Julai.

‘Tunayo furaha kutangaza ubia wetu na Tatu Mzuka kwenye kampeni hii. Kwa wale ambao mnatumia MPESA kucheza Tatu Mzuka mbali na kushuhudia timu yako ikishinda nchini Urusi, utaweza kushinda bidhaa mbalimbali, fedha, muda wa bure wa maongezi na intaneti kila unapocheza Tatu Mzuka kila siku’ alisema Bwana Ndekana

Kama nyongeza ya kampeini ya SupaMzuka Cup, Tatu Mzuka pia inadhamini urushaji wa matangazo ya Kombe la dunia kupitia TBC 1 na TV1 ili kuhakikisha kwamba Watanzania wote wanapata fursa ya kutazama michuano hii yenye mvuto.

No comments:

Post a Comment

Pages