HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 14, 2018

Tigo Yazindua Kampeni mpya ya ‘Tigo Pesa ni Zaidi ya Pesa’

Dar es Salaam, Tanzania

Tigo Pesa, Huduma ya Kifedha ya Kampuni ya Tigo Tanzania, imezindua kampeni ya ‘Tigo Pesa ni Zaidi ya Pesa’, kama uthibitisho kuwa huduma hiyo sasa ina hadhi ya huduma kamili ya kifedha ambayo inawapa wateja huduma za kipekee, bora na  nyingi zaidi kupitia mtandao wa simu.

Tigo Pesa ni Zaidi ya Pesa’ inazingatia sifa ya Tigo kuwa mtandao pekee unaobuni huduma na bidhaa kulingana na mahitaji ya wateja ili kuboresha na kurahisisha maisha yao.

‘Tigo Pesa imepanua wigo wa bidhaa na huduma zake na kuibua njia bora zaidi kwa wateja kufurahia huduma za haraka, uhakika na salama za kifedha popote walipo nchini Tanzania,’ Hussein Sayed, Afisa Mkuu wa  Huduma za Kifedha wa Tigo aliwaambia waandishi wa habari.

Kama sehemu ya kampeni hii, Tigo Pesa inajivunia kuwa mtandao pekee na wa kwanza wa simu unaotoa huduma inayowezesha wateja wa Tigo kurudisha miamala ya fedha zilizotumwa kimakosa kwenda kwa wateja wenzao wa Tigo.  Huduma hiyo inayopatikana kupitia menu ya Tigo Pesa  *150*01# inawapa wateja wa Tigo uwezo wa kurudisha kwa haraka miamala yoyote ya kutuma hela ikiwa watagundua kuwa wamekosea miamala hiyo, bila ya kuhitaji msaada wa moja kwa moja kutoka kitengo cha huduma kwa wateja.

‘Huduma hii ya kipekee ya kurudisha miamala iliyokosewa kwa haraka inajibu mahitaji ya wateja wengi ambao kwa sababu moja au nyingine wanafanya makosa pindi wanapotuma pesa. Ni huduma ya aina yake ambayo inawapa wateja uwezo zaidi juu ya miamala wanayofanya na imeundwa kwa kuzingatia vigezo vya hali ya juu vitakavyozuia matumizi mabaya ya huduma hii,’ Hussein alifafanua

Hivi karibuni, Tigo Pesa ilifungua ukurasa mpya wa maisha yasiyotegemea pesa taslim nchini, baada ya kuwa kampuni ya simu ya kwanza na pekee kuzindua huduma ya Tigo Pesa Masterpass QR. Huduma hii inawezesha wateja kulipia huduma na bidhaa haraka, kwa urahisi na usalama zaidi kwa njia ya kuscani nembo ya Masterpass Quick Response inayopatikiana katika maeneo tofauti ya manunuzi/huduma.

Tigo pia imeingia katika ushirikiano wa kipekee na kampuni ya teknologia ya Uber yanayowezesha wateja wa Tigo kutumia huduma za usafiri za Uber kwa bei ya punguzo na bila gharama za data. Ushirikiano huu ni muhimu kwa madereva na wasafiri wa Uber kwani unawezesha wateja zaidi kutumia Uber App kupitia simu zao na kupata usafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa urahisi na kwa bei ya punguzo. Kupitia Tigo Pesa pekee, wateja wa Tigo pia wana fursa ya kupata usafiri wa Uber bure kila mara wanapofanya miamala ya fedha kati ya akaunti zao za benki na akaunti zao za Tigo pesa. 

Tigo Pesa ndio huduma ya kifedha kwa njia ya mtandao inayokuwa kwa kasi zaidi nchini, ikiwa na wateja waliosajiliwa zaidi ya milioni saba, mtandao wa waanya biashara (merchants) zaidi ya 40,000 na mawakala zaidi ya   85,000 walioenea kote nchini.

Tigo ndio kampuni inayoongoza maisha ya kidigitali katika soko la mawasiliano ya simu nchini kwa miaka mingi. Tigo Pesa ndio huduma ya kwanza ya fedha kutoa gawio la faida kwa wateja wake. Tigo pia iliongoza juhudi za kuunganisha mitandao ya simu na mabenki ili kuunda mfumo wa kwanza duniani wa kifedha baina ya mabenki na mitandao ya simu. Mfumo huu umeongeza idadi ya miamala pamoja na kukuza ongezeko la idadi ya watu wanaotumia huduma rasmi za kifedha nchini.  Tigo pia ilikuwa kampuni ya kwanza ya simu za mkononi nchini na Afrika Mashariki kutoa huduma inayowezesha wateja kutuma na kupokea pesa kutoka nchi moja hadi nyingine kwa thamani ya sarafu ya nchi husika, hivyo kurahisisha na kuongeza wigo wa huduma za uhamishaji fedha baina ya nchi.

‘Kupitia kampeni ya ‘Tigo Pesa ni Zaidi ya Pesa’, Tigo inawaalika kutathmini hatua kubwa ambazo Tigo pesa imepiga katika kipindi hiki cha miaka michache. Kampeni hii pia inamkaribisha kila mtu kujiunga katika safari hii ya kipekee itakayowawezesha wananchi na biashara nyingi zaidi kuongeza idadi ya wanaotumia huduma rasmi za kifedha, kuboresha mazingira ya kidigitali na kufungua ukurasa upya wa maisha yasiyotegemea pesa taslim,’’ Hussein alibainisha.

No comments:

Post a Comment

Pages