HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 18, 2018

SPORTPESA YACHEZESHA DROO YA 28 NA KUTANGAZA ONGEZEKO LA ZAWADI

Kampuni ya mchezo wa kubashiri ya SportPesa imechezesha droo ya 28 ya Promosheni ya Shida Zaidi na SportPesa, ambapo Ndugu Amri Nicolas Juma (28) kutoka Kigoma ameibuka mshindi wa Bajaji RE.

Droo hiyo iliyooongozwa na Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti SportPesa Tanzania Ndugu Tarimba Abbas alitangaza ongezeko la zawadi kwenye promosheni hiyo, aambapo mbali na wachezeji wa SportPesa kupitia mitandao yote wananafasi ya kushinda Bajaji, na kuna zawadi mpya amnazo ni Smartphones, Jezi za timu ya Simba ama Yanga na Tiketi ya kuhuduria mechi za ligi ya Hispania na Uingereza kila mwezi.

Akizungumza na waandishi wa habari Ndugu Tarimba Abbas alisema” Kutokana na ukubwa wa promosheni yetu tumeona si haba endapo tukaongeza zawadi zitakazotolewa kila wiki na kila mwezi kwa wateja wetu ili kuwahamasisha waweze kushiriki na kushinda zawadi mbalimbali”

“Kila wiki tutawazawadia washindi kumi na nne jezi pamoja na simu za mkononi yaani Smartphones na kila mwezi tutawazawadia washindi wawili tiketi ya kuweza kuhudhuria mechi ya Ligi zinazoendelea Hispania pamoja na Uingereza”

“Ningependa kuwahamasisha watumiaji wa mitandao yote ya simu kushiriki vilivyo kwenye promosheni hii ili kuweza kujishindia zawadi mbalimbali kila siku.

“Mpaka sasa tumepata washindi kutoka zaidi ya mikoa kumi 13 Tanzania ambayo ni Dar es Salaam, Kigoma, Mwanza, Tanga, Singida, Ruvuma, Morogoro, Iringa, Kahama, Songwe, Mbeya, Pwani, na Lindi.

Hakuna kulala Mtanzania SportPesa wametuletea Bajaji mia moja cha kufanya kupitia simu yako ya mkononi ni kupiga *150*87#, kisha usisahau kuweka pesa kwenye akaunti kupitia mitandao ya simu ya mkononi na kuweka ubashiri wako moja kwa moja ili kuingia kwenye droo na kujishindia zawadi mbalimbali, kwa tovuti www.sportpesa.co.tz

No comments:

Post a Comment

Pages