Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa Tamasha
la Michezo na Maonesho ya Vyuo vya Ufundi
yaliyozinduliwa leo katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Chuo cha Veta Kanda ya Kati mara baada ya uzinduzi wa tamasha la michezo na maonyesho ya vyuo vya ufundi yanayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma, wa pili kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Ajira Kazi Vijana na Walemavu, Anthony Mavunde. (Picha na Maelezo).
Na Anitha Jonas –
WHUSM
Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mheshimiwa Dkt. Harrison Mwakyembe amewaahidi
viongozi wa Veta kufikisha vilio vya
changamoto zao kwa viongozi husika.
Mheshimiwa Mwakyembe
ameyasema hayo leo jijijni Dodoma
alipokuwa akizindua Tamasha la Michezo na Maonesho ya vyuo vya ufundi Kanda ya Kati Dodoma,mara
baada ya viongozi hao kusoma risala yao kuhusu tamasha lao ambalo litadumu kwa
wiki nzima lengo likiwa ni kujenga umoja na kuboresha mahusiano kwa vyuo
vya ufundi pamoja na kuweka mikakati ya
kutoa elimu bora yenye kusaidia taifa kufika malengo ya uchumi wa Kati na nchi
ya viwanda.
“Kwanza ninawapongeza
sana kwa kutambua umuhimu wa michezo katika kuwajenga vijana wenye ujuzi ambao
wanaelewa thamani ya michezo kwani michezo ni afya na michezo ni ajira kwa hakika jambo hili mlilolifanya ni
jambo zuri na pia natoa rai kwenu
wanamichezo wote mnaoshiriki michezo hii kucheza kwa amani ,“alisema
Mhe.Dkt.Mwakyembe.
Akiendelea kuzungumza
katika uzinduzi wa tamasha hilo Mhe.Mwakyembe alisisitiza kuwa katika
mashindano hayo asingependa kusikia kuwepo kwa wachezaji mamluki ambao siyo
wanamichezo kutoka katika vyuo husika vilivyoshiriki tamasha hilo.
Pamoja na hayo nae Naibu
Waziri Ofisi ya Mkuu Ajira Kazi Vijana na Walemavu Mhe.Anthony Mavunde alieleza
mipango mbalimbali serikali iliyojiwekea ya
kushirikiana na VETA kwa ajili ya kuhakikisha inawasaidia vijana kupata mafunzo ya ufundi ambayo yatawawezesha
kujiajiri na kufanikisha adhima ya nchi yetu kufikia uchumi wakati na nchi ya
Viwanda.
“Kupitia umoja huu wa
vyuo vya ufundi kwa kanda ya kati waliyouanzisha nitajitahidi kuwasimamia na
kuhakikisha wanaanzisha kiwanda chao wenyewe cha mfano ,“Mhe.Mavunde.
Aidha,nae Kaimu Mkuu
wa Chuo Veta Kanda ya Kati Bw.Ramadhan Mataka alieleza kuwa VETA kama wasimamizi
wa vyuo vinavyotoa mafunzo ya ufundi nchini hivi karibuni uongozi wa Kanda ya
Kati imevifungia vyuo ishirini vilivyokuwa havina viwango vya kutoa mafunzo
kukuzingatia sheria na utaratibu wa hadhi ya vyuo vya ufundi.
“Kupitia Umoja wa Vyuo vya Ufundi tunataka
tuunde mkakati madhubuti wa kuboresha kozi zetu na kuhakikisha tunatoa mafunzo
yenye ubora ambayo yatatusaidia wote
kutembea katika njia moja kwa manufaa ya taifa letu na uchumi wa nchi yetu,”Bw.Mataka.
Sambamba na hayo Bw. Mataka alitoa rai kwa vyuo vyote vya
ufundi vilivyopo Kanda ya Kati ambavyo havijasajiliwa vijisajili haraka ili
kurasimisha shughuli zao,”Bw.Mataka
Halikadhalika nae
Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Vyuo vya Ufundi Dodoma, Bw.Jeremia Philip alieleza kuwa umoja huo unamalengo
mbalimbali ikiwemo kuboresha masomo ya mafunzo ya ufundi na kuwaongezea vijana
ujasiri wa kujiajiri mara baada ya kufuzu masomo yao.
Pamoja na hayo Bw.Jeremia alieleza kuwa umoja
huo umeanzisha mpango wa kurudisha darasani vijana ambao hawakupata elimu
waliyochini ya miaka kumi na tano wa kuwapeleka darasani na kuwapatia mafunzo ya ufundi kwa lengo la
kuwasaidia kuweza kujikwamua kiuchumi.
No comments:
Post a Comment