HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 06, 2018

Halotel kuwazawadia wateja na Chrismas BANG BANG

 Mkuu wa mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda akizungumza na waandishi wa Habari katika Makao Makuu ya kampuni hiyo kuhusu Ofa mpya ya Krismasi na mwaka Mpya iliyozinduliwa leo inayokwenda kwa jina la “Christmas Bang Bang” namna itakayowawezesha wateja wote wa Halotel kupata GB2 za intaneti kwa sh. 2000 tu.na pia wateja wote watapata zawadi wataaakapofika maduka yetu yote nchi nzima. Pamoja nae katika picha kushoto ni Meneja Mawasiliano Halotel, Hindu Kanyamala na kulia ni Meneja Uhusiano wa kampuni, hiyo Stella Pius.
Mkuu wa Mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu Ofa mpya ya Krismasi na mwaka Mpya inayojulikana kwa jina la “Christmas Bang Bang”, ambayo itawawezesha wateja wote wa Halotel kupata GB2 za intaneti kwa sh. 2000. Kulia ni Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Stella Pius.

NA FRANCIS DANDE

KATIKA kuelekea msimu wa Sikukuu Kampuni ya simu ya Halotel imetoa punguzo la zaidi ya asilimia sitini (60%) katika kifurushi chake cha siku ambapo sasa wateja watapata GB 2 kwa shilingi 2000 ikiwa ni gharama nafuu zaidi ya vifurushi vya intaneti na kutoa punguzo kubwa la smartphone aina ya OXE 101.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu punguzo hilo kubwa, Mkuu wa Mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda, alisema ofa hiyo imezingatia mahitaji makubwa ya wateja wa mtandao huo katika msimu huu wa sikukuu na kutoa nafasi kwa wateja kupeana taarifa na fursa ya kutembelea mitandao mbali mbali ya kijamii.

“Msimu wa sikukuu unatoa fursa kwa wateja wetu, kutembelea maeneo mbalimbali ya nchi, wengi wanahitaji taarifa za maeneo wanayoenda, au wanaweza kupenda kushare matukio au hata kupata muda mwingi wa kutumia simu zao, hivyo tumeonelea ni vyema sasa, tuwape sababu ya kufurahia msimu huu wa sikukuu kwa kuwapatia ongezeko kubwa kabisa la GB za intaneti”, alisema Mhina na kuongeza.
 
Jambo kubwa kabisa la kuwahakikishia wateja wetu ni kuwa maeneo yote watakayo kwenda iwe vijijini au sehemu nyinginezo, watakuwa pamoja nasi na watakuwa na uhakika wa kutumia huduma zetu kutoka katika mtandao wetu uliosambaa Zaidi hapa nchini kwa kufikia Zaidi ya asilimia 95% ya Watanzania.

“Huduma hii ni zawadi kwa wateja wote wa Halotel nchini msimu huu wa sikukuu kwa kuendelea kutumia intanet yenye kasi zaidi nchini kipindi hiki cha mapumziko wakati wowote, ambapo kwa kujiunga na huduma ya CHRISTMAS BANG BANG mteja atapata kifurushi cha intenet cha GB 2 cha siku kwa sh 2000 tu tofauti na kirushi cha kawaida ambacho mteja angepata GB 1.3 kwa siku kwa sh 2000.

 Zaidi tunapenda kuwakumbusha watanzania na wateja wetu wote wataweza kujipatia zawadi mbali mbali pindi watakapo fika kwenye maduka yetu ya Halotel nchi nzima katika kipindi msimu huu wa sikukuu. Tunatakia watanzania na wateja wa Halotel waipokee zawadi ya CHRISTMAS BANG BANG kutoka Halotel, alisema Semwenda na kuongeza.

Tunawahakikishia wateja wetu kuwa tutafanya msimu huu wa sikukuu kuwa Bang Bang kwa kuendelea kuboresha huduma zetu.

No comments:

Post a Comment

Pages