HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 08, 2018

Mashirika ya Umoja wa Matifa Yaadhimisha ya Siku 16 za Kupambana na Udhalilishaji wa Wanawake na Watoto

Na Talib Ussi, Zanzibar
Umoja wa mataifa  (UN) imeeleza inawezekana kuwa na taifa bila ya udhalilishaji wa wanawake na watoto, jambo ambalo ni kero kubwa katika jamii mbali mbali Tanzania na Duniani kote.
Akizungumza kwa niaba ya mashirika ya UN katika maadhimisha ya siku 16 za kupambana na udhalilishaji wa wanawake na watoto zilizofanyika Visiwani Zanzibar katika Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul-Wakili, Alvaro Rodriguez (Pichani),  alisema inasikitisha kuona kwamba bado katika jamii nyingi Duniani udhalilishaji unaendelea.
“Tunaweza kutokomeza vitendo hivi viovu kwa kila mmoja kutekeleza wajibu wake , tuungane ili akina mama waishi bila ghofu” alisema Rodregues alisema tamko la Un kuhusiana na siku 16 kupinga ukatili wa kijinsia.
Alieleza kuwa maendeleo ya wanawake hayawezi kufikiwa ikiwa jamii zilizonguka bado zinaendelea na udhalilishaji.
“Udhalilishaji hauvumiliki ni lazima tutapambane nao kwa hali yoyote ile kwa maslahi ya jamii iliyobora” alieelza mwakilishi huyo wa un.
Aidha aliomba jamii kuwafariji wahanga wa vitendo hivyo na kuchukuliwa hatua kali kwa wahalifu wanaotenda vitendo hivo.
Kwa upande wake Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi zanzibar  Balozi Seif Ali Idd amewataka wanawake kutokuogopa kuachwa na waume zao (kupewa talaka) kwa kuwaficha wahalifu wa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia.
Balozi alieleza kuwa wapo baadhi ya wanwake kutotoa taarifa au kuwaficha wadhalilishaji kwa kuogopa kuachwa au kupewa talaka na waume zao jambo linasababisha vita dhidi ya udhalilishaji kuwa ngumu.
“Kama mwanamke ukificha vitendo vya udhalilishaji basi mtoto wako akiendelea kufanyiwa udhalilishaji usipige kelele, ni vyema sote tukashirikiana kuliondoa janga hili” alieleza Balozi Seif.
Sambamba na hilo Balozi alieleza kuwa kutokomeza kabisa jambo hilo ni lazima kuwepo nguvu ya pamoja baina ya jamii, Wanasheria pamoja na Serikali.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Vyama vya Wafanyakazi zanzibar Khamis Mwinyi Muhammed alisema taasisi yake imekuwa ikipiga siku zote suala la udhalilishaji.
“Tulinde nguvu kazi tumalize udhalilishaji wa kijinsia sehemu za kazi” alieelza katibu huyo ambao huo ni ujumbe mwaka huu.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya ya Kazi, Uwezeshaji Wazee wanawake na Watoto zanzibar Bi Fatma gharib Bilali alisema wazara yake imezifanyia mabadiliko sheria nyingi ambazo zinahusiana na vitendo hivyo kwa lengo kuziba mwanya wa kutokea kwa watendaji wa laana hiyo.
Alieleza kuwa katika sheria ya ajira  namba 11 ya 2015 imewataka taasisi binafsi kupambana na udhalilishaji katika maeneo yao ya kazi.
“Tumeamua kufanya sheria kali ili kuwadhibiti wahalifu wa vitendo hivi na kwa sasa hawatakiwi kupewa dhamana”  alieleza Bi Fatma.
Dunia huazimisha siku 16 kila mwaka  kwa lengo la kuongoza mwamko wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji.

No comments:

Post a Comment

Pages