HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 21, 2020

Mabadiliko mbio za ‘Relay’ Taifa

MASHINDANO ya Mbio za Kupokezana Vijiti ‘Relay’ Taifa yaliyokuwa yafanyike kesho Jumamosi Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, sasa yamesogezwa mbele hadi keshokutwa Jumapili.

Sababu za kusogezwa mbele kwa siku moja mashindano hayo, ni kutoa nafasi kwa wachezaji kufika jijini Dar es Salaam, baada ya baadhi yao kukabiliwa na changamoto ya usafiri, ambapo wengi wao watafika Jumamosi.

Mashindano hayo yatashirikisha mbio za mita 100X4 na 400X4 yakishirikisha wanariadha kutoka mikoa tisa waliofikia viwango maalumu vilivyowekwa na Kamati ya Ufundi ya Shirikisho la Riadha Tanzania (RT).

Mashindano hayo, yanafanyika baada ya mikoa mbalimbali kuendesha mashindano ‘Trials’ na wale wanariadha waliofikia viwango vilivyowekwa na Kamati ya Ufundi ya RT, ndio wanakutana katika fainali Jumapili.

 “Tunaamini viongozi wa mikoa wamezingatia viwango tulivyotoa na hakuna udanganyifu, hivyo tunategemea ushindani utakuwa mkubwa sana na tutapata timu nzuri,”.

Tunawaomba wadau na wapenzi wa michezo, kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa Jumapili kushuhudia mbio hizo na kuwapa hamasa wachezaji, kiingilio ni bure.

Wanariadha watakaoshiriki na wanakotoka kwenye mabano ni Winfrida Makenji, Emmy Hosea, Ali Khamis Gulam, Hassan Khamis Ali, Naima Ali Musa, Abdallah Issa Khamis , Mohammed Ali Mshamba na Simai Kombo Haji (Zanzibar).

Wengine ni Binamunzi Katunzi, Ismail Tossil na Diana Matemu (Dodoma), Daniel Mussa, Elisha Machungwa, Japhet Kitungu (Mara), Boniface Inalo, Benjamin Michael, Jumanne Chacha, Andrea Robi (Arusha), Elias Sylvester, Selemani Sabin a Jeremiah Baruti (Dar es Salam).

Pia wamo Ramadhan Omary, Fahadi Juma, Petro Joseph (Singida), Jacob Lugaila (Mwanza), Bora Hassan (Tabora), Matondo Magembe, Rose Lucas, Thereza Benard, Rahel Nilla (Simiyu), Benedictor Mathias, Regina Mpigachai, Pili Mipawa, Amos Charles (Pwani), Elias Sylvester, Selemani Sabi na Jeremiah Baruti (Dar es Salaam).

IMETOLEWA NA:
Tullo Chambo
Msemaji RT
0752 46 21 03
21 /FEBRUARI/ 2020

No comments:

Post a Comment

Pages