Hayati Bibi Titi Mohamed.
NA MWANDISHI WETU
WATANZANIA
mbalimbali wamealikwa kujitokeza kuchangia ujenzi wa shule maalum ya
Sekondari itakayoitwa Bi.Titi Mohamed kwa ajili ya kumuenzi mpigania
Uhuru Mwanamama ambaye pia alikuwa mbunge wa kwanza Jimbo la Rufiji.
Kwa mujibu wa taarifa kwa Umma ya mwaliko huo iliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Lt. Col Patrick Sawala imeeleza kuwa:
"Tunawaalika
wadau na watu mbalimbali kujitokeza kwenye Harambee ya kuchangia ujenzi
wa shule ya Sekondari Bi. Titi Mohamed, 27 February kuanzia majira ya
Sita mchana hadi Saa 12 jioni Katika Ukumbi wa SabaSaba ndani ya viwanja
vya Sabasaba, barabara ya Kilwa, Jijini Dar es Salaam" Ilieleza
taarifa hiyo.
Aidha,
mchango wa Harambee pia wadau na Wananchi wanaweza kuutuma kupitia:
Benki ya NMB yenye jina la Maendeleo Kata ya Ngorongo akaunti namba
21310024867.
Pia michango
inaweza kutumwa kwa njia ya mtandao wa simu wa Tigo Pesa namba
0716480956 yenye jina la Sikujua Gallusy Mavika". alieleza mkuu wa
Wilaya kwenye taarifa hiyo.
Aidha
shule hiyo inatarajiwa kujengwa kwa nguvu za Wananchi, wadau wa
Maendeleo, na Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji hili ni kuunga mkono
juhudi za Serikali ya awamu ya Tano katika kuhakikisha kila mtoto mwenye
sifa ya kwenda shule anaenda shule bila kikwazo na bila malipo yoyote.
Akifafanua
zaidi, alisema ghalama za awali kwenye ujenzi wa shule hiyo ni zaidi
ya Tshs Milioni 550. Hivyo wanatarajia kukusanya Tshs. Bilioni moja
ilikukamilisha ujenzi wake kiujumla.
Hata
hivyo wananchi na Wadau wanaweza pia kuchangia fedha taslimu au vifaa
vya ujenzi moja kwa moja kwa ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Rufiji.
Katika tukio hilo, wadau mbali mbali wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Serikali na wageni waalikwa watashiriki.
No comments:
Post a Comment