Mabondia Chipukizi Wilaya Ya
Ubungo Waonesha Umwamba Wa Mchezo Wa Masumbwi Kuwania Nafasi Ya Kucheza
Pambano La PayBack Night kati Ya Dulla Mbabe Dhidi Ya Eric Katompa
Julai 15,2023 Dar es salaam.
Wakizungumza Mabondia mara Baada ya kuibuka Washindi wa Mapambano yao Yaliyofanyika katika Viwanja Vya Kifa Mburahati Wamesema Haikuwa Rahisi Kupata nafasi ya kuonesha nguvu ya vipaji vyao huku wakishukuru kupata nafasi ya Kucheza Pambano kubwa la kimataifa na Kuahidi Watanzania kuona Burudani Mpya Yenye Utalaamu Wa Ngumi Kutoka Mtaani Siku hiyo.
Kwaupande wao Mabondia waliopoteza Mapambano hayo Wamesema Licha Ya Kutokufanya Vizuri Wameshukuru kupata nafasi ya kuonesha uwezo wao na ni njia moja wapo yao kufanya vizuri katika Mchezo wa ngumi Tanzania.
Mabondia Waliofanya Vizuri kwenye mashindano hayo wamepata nafasi ya kumsindikiza Bondia Mtanzania Dulla Mbabe katika Pambano la Marudiano na Erick Katompa Wa Kongo huku Nassibu Ramadhani kumaliza utata na Loren Japhet, Ramadhani Iddi kuzichapa na Peter Toshi Wa Mbweni JKT, Hassan ndonga na Tasha mjuaji Katika Pambano la Kisasi Julai 15, 2023 kwenye Uwanja Wa Kinesi Jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment