HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 09, 2023

MABONDIA CHIPUKIZI UBUNGO NI ZAIDI YA TEMEKE NA KINONDONI

Mabondia Chipukizi Wilaya Ya Ubungo Waonesha Umwamba Wa Mchezo Wa Masumbwi  Kuwania Nafasi Ya Kucheza Pambano La PayBack Night kati Ya Dulla Mbabe Dhidi Ya Eric Katompa Julai 15,2023 Dar es salaam.

 

Wakizungumza Mabondia mara Baada ya kuibuka Washindi wa Mapambano yao Yaliyofanyika katika Viwanja Vya Kifa Mburahati  Wamesema Haikuwa Rahisi Kupata nafasi ya kuonesha nguvu ya vipaji vyao huku wakishukuru kupata nafasi ya Kucheza Pambano kubwa la kimataifa na Kuahidi Watanzania kuona Burudani Mpya Yenye Utalaamu Wa Ngumi Kutoka Mtaani Siku hiyo.

 

Kwaupande wao Mabondia waliopoteza Mapambano hayo Wamesema Licha Ya Kutokufanya Vizuri Wameshukuru kupata nafasi ya kuonesha uwezo wao na ni njia moja wapo yao kufanya vizuri katika Mchezo wa ngumi Tanzania.

 

Mabondia  Waliofanya Vizuri kwenye mashindano hayo wamepata nafasi ya kumsindikiza Bondia Mtanzania Dulla Mbabe katika Pambano la Marudiano na Erick Katompa Wa Kongo huku Nassibu Ramadhani kumaliza utata na Loren Japhet, Ramadhani Iddi kuzichapa na Peter Toshi Wa Mbweni JKT, Hassan ndonga  na  Tasha mjuaji Katika Pambano la Kisasi Julai 15, 2023 kwenye Uwanja Wa Kinesi Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages