HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 09, 2023

WANANCHI WATAKIWA KUENDELEA KUIAMINI SERIKALI

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba akisaini kitabu cha wageni katika banda la Wizara ya Fedha kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini humo. Kulia ni Katibu Muhtasi wa Wizara hiyo, Bi. Masia Msuya.


Na Farida Ramadhani, WF – Dar es Salaam

 

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba amewataka wananchi kuendelea kuiamini Serikali kwa kuwa mambo yote iliyoyapanga yatatekelezwa kikamilifu.

Ametoa rai hiyo alipotembelea na kuzungumza na washiriki wa banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba, Barabara ya Kilwa, jijini humo.  

Dkt. Mwamba alisema katika kipindi hiki cha utekelezaji wa Bajeti Kuu ya Serikali iliyosomwa hivi karibuni, Serikali itahakikisha inatekelezwa kiufasaha na kufukia malengo yaliyo kusudiwa.

Akizungumzia Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja vya sabasaba jijini humo, aliwahamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi ili kupata elimu kuhusu masuala mbalimbali ya biashara na uwekezaji.

 

“Hapa ni kwa ajili ya biashara, viwanda na uwekezaji, kuna mengi ya kujifunza ambayo yatawezesha wananchi kujiinua kiuchumi”, alibainisha Dkt. Mwamba.

Alisema katika banda la Wizara ya Fedha, washiriki wanaari ya kuwahudumia wananchi hivyo watakapo tembelea maonesho hayo wasisite kupitia banda hilo muhimu katika kusimamia uchumi wa nchi.

“Washiriki wamejipanga na kwa namna wanavyotoa elimu ni rahisi mno kuwaelewa na kufanya maamuzi sahihi kutokana na elimu iliyopatikana” alifafanua Dkt. Mwamba.

Aidha, alionesha kufurahishwa na namna ambavyo wananchi wameonesha kufurahishwa na kuondolewa kwa tozo za miamala ya simu na kubainisha kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha inapunguza maumivu kwa wananchi.



No comments:

Post a Comment

Pages