HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 14, 2023

Waziri Dkt. Kijaji ashuhudia utiaji Saini Mikataba 10 ya Kampuni za Uwekezaji Kimkakati

Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji ameshudia uwekaji wa saini mikataba ya makampuni kumi wenye hadhi ya  uwekezaji  wa kimkakati mahiri  wenye jumla ya  thamani ya Dola za Marekani Mil 1805.12  na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

Katika uwekezaji huo uliopewa hadhi hiyo na Kamati ya Taifa ya Uwekezaji (NISC) ni wa kwanza kushuhudiwa na  Kituo cha Uwekezaji (TIC) ambapo utatoa   kwa ajira za moja kwa moja 16,355 na ajira zilizokuwa za moja kwa moja 200,000.
Akizungumza wakati wa utiaji wa saini wa mikataba hiyo, Kijaji amezitaka taasisi hizo kupunguza na kumaliza kabisa changamoto ya Tanzania kuagiza bidhaa kutoka nje wakati uwezo wa kuzalisha hapa nchini upo.

Amebainisha kuwa Serikali imekuwa ikiongeza nguvu kwa wakulima, ilikuweza kuzalisha mali ghafi za kutosha zitakazoweza kuchakatwa na viwanda vya hapa hapa nchini na kuzalisha bidhaa zitakazouzwa ndani na nje ya nchi.

Kijaji amefafanua kuwa kama wanavyoenda kumaliza changamoto ya uagizaji wa sukari mwaka 2024, amezitaka kampuni za uchakati wa mafuta  kumaliza kabisa kilio cha Watanzania kuhusu changamoto ya uhaba  wa mafuta ya kupikia  ifikapo  mwaka 2027 kwa kuzalisha  mafuta tani 560,500 kutoka tani 205,000 yanayozalishwa sasa.

"Haina haja ya kuagiza mafuta kutoka nje, wakati wapo wakulima ambao wanalima mbegu za kukamua mafuta.

Kilio cha wawekezaji ilikuwa ni kuwepo kwa viwanda lakini wanakosa mali ghafi, kwa sasa Serikali imewekeza huko tukafaye kazi" alisema.

Ameongeza kuwa Serikali itazindua  mtandao wa kituo kimoja kwaajili ya mwekezaji kupata huduma zote sehemu moja, ili kumpunguzi  usumbufu wa kutembea na nyaraka katika kutafuta cheti.

Alisema huduma hiyo itaweza kuwasaidia wageni wakiwa huko huko kuomba vibari na kukamilika kwa siku tatu, ambapo haitakuwa na usumbufu kama ambao ulikuwa zikijitokeza mwanzo kutokana utofauti wa kanuni na kisheria na kufanya baadhi ya wawekezaji kushindwa kuwekeza.

"Nitaendelea kuwaambia kwamba Tanzania sio kisiwa kama tupo peke yetu, mwekezaji ukimsumbia anafanya kujadili na kwenda nchi zingine.

Kunasiku sio ghalama ni kuamua kwamba anahamisha, kwahiyo ni Jambo linalohitaji kuongea nao na sio kuwasumbua" alisema.

Katika mikataba hiyo waliokuja kusaini katika makampuni 10, sita ni kutoka nje ya Tanzania, watatu ni wawekezaji wa Tanzania ni mmoja anaubia wa Tanzania na sekta binafsi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Gilead Teri amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa kituo hicho kwa mara ya kwanza ameshuhudia utiaji wa saini wa  mikataba ya utekelezaji na makampuni kumi kwa wakati mmoja.

Pia amesema mikataba hii inaashiria mafanikio makubwa ya kihindi za uboreshaji wa Mazingira ya Uwekezaji, kuongezeka kwa ufanisi wa utiaji wa huduma kwa wawekezaji na kuimarika kwa juhudi za uhamasishaji Uwekezaji hapa nchini.

"Tunashukuru wawekezaji walioamua kuunganisha juhudi za Serikali kwa kuwaletea wananchi maendeleo na kukuza uchumi kupitia Uwekezaji" alisema.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Kuchakata Mafuta ya Wild Flower  Gran's Oil, Azizi Omary amesema wanatarajia kufikia kiwango hicho cha uchakataji wa mafuta kabla ya muda waliopanga Serikali.

Aidha amesema matarajio yao makubwa ni kuona kiwanda hicho kinatanuka zaidi kutoka mkoani  Singida kwenda Dodoma na mikoa mingine wanaozalisha mbegu za mafuta.

"Tumejipanga na uwekezaji huu kuhakikisha, tunachakata mafuta ya kutosha" amesema


No comments:

Post a Comment

Pages