Ndg .Baraka Musa, mgombea wa udiwani kata ya Kisarawe kupitia CHADEMA akichangia katika mdahalo huu uliowaohusisha wakazi wa kisarawe na wanafunzi.
NA MWANDISHI WETU, KISARAWE
WAGOMBEA udiwani wa Kisarawe wametakiwa kueleza namna
watakavyosaidia wanafunzi wa kata hiyo kuepukana na tatizo la usafiri kwa
kuwajengea mabweni.
Wakizungumza wakati wa kipindi cha redio cha ‘Walinde
Watoto’, kilichoandaa mdahalo uliowahusisha wagombea udiwani wa Kisarawe, Abel
Mudo (CCM), Baraka Musa (Chadema) na wakazi wa Kisarawe walijadili changamoto
zinazowakabili wanafunzi na mipango ya kuzitatua.
Amina Joka, mwanafunzi wa Shule ya Msingi Chanzige ‘A’ alisema
wanafunzi wanapata shida ya usafiri, hali inayowaathiri kitaaluma huku wazazi
na viongozi walioshiriki mdahalo huo wakitaka wagombea hao kuzingatia elimu kwa
watoto.
Akinadi Ilani ya Chadema, Musa alisema chama chao kinaamini
kuwa lishe bora ni muhimu kwa ustawi wa watoto kiafya na kielimu na kuahidi kuwekeza
kwenye kupata Katiba itakayotambua na kutaja haki za watoto.
Mudo wa CCM alisema endapo chama chake kitapata ridhaa ya
kuendelea kuongoza nchi kitawekeza katika shule na kuhakikisha zina walimu wa
kutosha na mazingira rafiki ya kujifunzia kwa wenye ulemavu.
|
No comments:
Post a Comment