- Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Ubungo, Evelyne Mushi (kushoto) akimkabidhi baba wa watoto pacha wanee, Abednego Andrew Mafuluka mkazi wa Kimara Mwisho, Dar es Salaam mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 ikiwa ni msaada kwa mapacha hao wanne. Benki ya NMB imewafungulia akaunti za watoto kwa kila mtoto na kuwawekea shilingi cha shilingi milioni 10, kuwasaidia wazazi na watoto hao hapo baadaye. Wa pili kulia ni mama mzazi wa mapacha hao, Sara Dimosso akiwa kabeba watoto wake huku akisaidiwa na nduguye.
- Baadhi ya maofisa wa Benki ya NMB wakiwa katika picha na familia ya Bwana na Bibi Abednego Andrew Mafuluka pamoja na watoto wao mapacha wanne mara baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya msaada.
- Bwana Abednego Andrew Mafuluka (katikati) akizungumza kuishukuru Benki ya NMB baada ya kuguswa na kuamua kuwasaidia watoto wao mapacha wanne.
- Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Ubungo, Evelyne Mushi (kushoto) akizungumza kuelezea namna Benki ya NMB ilivyoguswa na kuamua kuwasaidia watoto hao mapacha wanne waliozaliwa pamoja.
- Mama mzazi wa watoto mapacha wanne, Sara Dimosso (kulia) pamoja na mume wake, Abednego Andrew Mafuluka akizungumza kuishukuru Benki ya NMB kwa kuwasaidia shilingi milioni 10 iwawezeshe katika malezi ya watoto hao.
- Baadhi ya maofisa wa Benki ya NMB wakiwa katika picha na familia ya Bwana na Bibi Abednego Andrew Mafuluka pamoja na watoto wao mapacha wanne mara baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya msaada.

No comments:
Post a Comment