HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 24, 2017

ALEX MSAMA APONGEZWA KWA KAZI NZURI YA KUPAMBANA NA UHARAMIA WA KAZI ZA SANAA JIJINI DAR ES SALAAM

Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama, Alex Msama amekishukuru Chama cha Wanamuziki (TAMUNET) na wanamuziki kwa ujumla kwa kutambua mchango wa kampuni yake na kutambua mchango wake binafsi kutokana na kazi anayoifanya ili kupunguza kazi haramu za musiki na filamu hapa nchini.

Msama ametoa shukurani hizo baada ya kupokea barua kutoka taasisi hiyo ya muziki ikimpongeza kwa kazi anayoifanya katika kuhakikisha hakuna CD feki za kazi za muziki na filamu hapa nchini huku , akisisitiza kuwa CD zote zinatakiwa kuuzwa huku zikiwa na stika za TRA na mtu yeyote atakayeuza CD zisizo na stika za TRA atakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria, Pitia barua iliyotumwa kutoka chama cha Tanzania Musicians Network kwenda kwa Msama hapa chini.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya kupokea barua ya pongezi kutoka Chama cha Wanamuziki Tanzania (TAMUNET), Pia Msama alizungumza zoezi la kuwakamata watu wanaojihusisha na wizi wa kazi za wasanii katika eneo la Tegeta.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu zoezi la kuwakamata wafanyabiashara wa CD feki pamoja na wale wanaoingiza nyimbo za wasanii katika simu katika maeneo ya Tegeta.
NSAMA3

No comments:

Post a Comment

Pages