HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 29, 2020

KALIUA IMENUNUA BANDALI 300 ZA BATI YA KUKAMILISHA MABOMA YA SHULE


Na Tiganya Vincent

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kaliua katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Machi imenunua bandali 300 kwa gharama ya milioni 80 kutokana na mapato ya ndani.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Haruna Kasele wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.
Alisema bati hizo zitagawanywa katika Kata zote ambazo zimekamilisha mabona, ununuzi wa mbao na vifaa kwa ajili ya upauaji.

Aidha , Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa wanaendelea na ujenzi wa vyumba 6 vya maabara katika shule za sekondari ya Kanoge, Kamsekwa, Zugimulole, Silambo, Seleli na Ilege.

Katika hatua nyingine Kasele alisema Kaliua imeshapokea shilingi bilioni 1 kwa ajili ya mpango  wa elimu bila malipo kutoka Serikali kuu. 

Alisema kwa upande wa shule za Msingi wamepokea shilingi milioni 683.9 na shule ya sekondari wamepokea shilingi milioni 399.8.

Kasele aliishukuru Serikali kwa kutoa fedha hizo ambazo zimewawezesha wanafunzi kujiunga na Shule za Msingi na Sekondari katika uongozi wa awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wakati huo huo Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua imetoa jumla ya mikopo ya shilingi milioni 345 kwa vikundi mbalimbali.

Kasele alisema shilingi milioni 133.5 zimetolewa kwa vijana, shilingi milioni 184 zimetolewa kwa wanawake na milioni 27.5 zimetolewa kwa walemavu.

Alivitaka vikundi ambavyo vimekopeshwa kuhakikisha wanarejesha fedha hizo ili ziweze kukopeshwa kwa vikundi vingine.

No comments:

Post a Comment

Pages