KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Taifa, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, amemtaja Rais Samia Suluhu
Hassan, kuwa turufu ya maendeleo ya Watanzania kutokana na falsafa
iliyobeba mambo matatu anayoyatumia katika uongozi wake.
Mambao hayo ni upangaji, usimamiaji na utekelezaji.
Shaka
aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akipokea tuzo ya
kumpongeza Rais Samia kwa utendaji mzuri, iliyotolewa na Umoja wa Vijana
wa CCM (UVCCM), Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Alisema
Rais Samia amekuwa turufu ya maendeleo ya watanzania kutokana na
falsafa tatu anazozitumia katika uongozi wake ambazo ni upangaji,
utekelezaji na usimamiaji.
Kwa mujibu wa Shaka, hayo yamejidhihirisha katika uongozi wake kwa kipindi cha miezi tisa ambapo mambo makubwa yamefanyika.
Alieleza
katika kipindi hicho umeshuhudiwa utekelezaji mkubwa wa Ilani ya
Uchaguzi ya CCM mwaka 2020-2025, kwamba wanaamini kufikia mwaka 2025
utekelezaji utazidi asilimia 100.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Tawi la UDSM, Isack Sambuli, alisema
uamuzi wao huo unatokana na kuguswa na mambo makubwa anayoyafanya Rais
Samia ambayo moja kwa moja yanawagusa wanafunzi wa elimu ya Juu na
Watanzania kwa ujumla.
Alisema miongoni mwa mambo hayo makubwa ni pamoja na kuongeza fedha kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya Juu.
Sambuli
alisema uamuzi wao huo haukulenga kutaka kutazamwa kwa ajili ya uteuzi
wa uongozi Bali wamelenga kutazama uhalisia wa mambo makubwa.

No comments:
Post a Comment