Imeelezwa kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan inathamini mchango wa Madhehebu ya dini kupitia mahubiri na kufundisha neno la Mungu kwa watu wote.
Hayo
 yamebainishwa na Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko katika Maadhimisho 
ya Jubilee ya Miaka 75 ya Kanisa la Elimu Pentekoste Tanzania (KEPT) 
iliyofanyika Wilaya ya Babati mkoani Manyara.
Akizungumza
 kwa niaba ya Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango, Dkt. Biteko 
ametoa pongezi kwa niaba ya Serikali kwa mambo yanayofanyika ya kuhuburi
 kwa watu na Taifa kwa ujumla ikiwemo kufundisha neno la Mungu kwa watu 
wote.
Pia, amewapongeza 
kwa kutoa huduma za kijamii ikiwemo elimu na afya, kuendelea kuhimiza 
waumini wote kudumisha amani, upendo, mshikamano na utulivu kwa kufanya 
kazi kwa bidii pamoja na kutunza mazingira.
Dkt.Biteko
 amesema, Mhe. Rais Samia ameendelea kusisitiza kuwahudumia watanzania 
kwa heshima kubwa ili maisha yao yazidi kuwa bora kila wakati.
"Nitoe
 mfano kwa sekta ninayoiongoza ya Madini, tangu Mhe.Rais ameingia 
madarakani ametuelekeza kufuta baadhi ya kodi mbalimbali ambazo 
wachimbaji wadogo walikuwa wanaona ni kero katika shughuli zao.
Pia,
 Mhe. Rais amesisitiza kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji wa 
ndani na nje kwa kufuta baadhi ya vipengele vya Sheria na Kanuni ambavyo
 vilikuwa vinakwaza uwekezaji.
"Yote
 haya, Mhe. Rais anayafanya kwa sababu kiu yake ya kuona kila mwananchi 
ndani ya nchi hii anakuwa na furaha na maisha yake, na kufurahia kufanya
 kazi anayoifanya kwa ajili ya kuendeshea maisha yake," amesisitiza Dkt.
 Biteko.
Aidha, Dkt. 
Biteko kwa niaba ya Makamu wa Rais ameshiriki katika uwekaji wa jiwe la 
msingi wa ujenzi wa jengo la kanisa na upandaji wa mti wa kumbukumbu.
Kwa
 upande wake, Baba Askofu Mkuu wa KEPT, Peter Konki amesema, kanisa 
lilianzishwa na Wamisionari kutoka Uingereza mwaka 1946 nchini Tanzania.
Amesema,
 walifungua makanisa ya kwanza wilaya ya Kondoa mkoa wa Dodoma, Msolwa 
katika mkoa wa Pwani, Tanga na wilaya ya Babati Mkoani Manyara.
Askofu
 Konki ametoa wito kwa jamii na watanzania kushiriki katika kudumisha 
amani na utulivu iliyopo kwa vitendo na kuendelea kufanya kazi kwa bidii
 na kuishi maisha mema.
Hafla
 ya Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 75 ya KEPT imehudhuriwa na Naibu 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la 
Babati, Pauline Gekul, Maaskofu Wakuu kutoka Madhehebu mengine na 
waumini mbalimbali.

No comments:
Post a Comment