Na Mwandishi Wetu
Waoka mikate wa Azam FC wamechomoza na ushindi wa bao (1-0) dhidi ya Simba SC, mchezo wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (NPL)
Ulikuwa na mchezo bora kwa timu zote katika dakika zote 90 za mpambano huo.
Azam FC walikuwa bora sana eneo la katikati mwa uwanja chini ya Issah Ndala, James Akaminko na Kenneth Mgunda wakati ambao Simba waliwakosa Mzamiru Yassin na Sadio Kanoute.
Azam FC wamejipatia bao lao kupitia kwa Prince Dube kipindi cha kwanza bao lililodumu hadi kipyenga cha mwisho cha Ramadhan Kayoko.
.jpeg)
Simba wamestahili kupoteza mechi ya leo kwa kiwango walichokionyesha wakati Azam wangeweza kufunga zaidi ya mabao mawili kama wangekuwa na umakini katika eneo la mwisho, ni ngumu kushinda mechi ya mpira wa miguu kama unakosa ufanisi katika kufanya vitu vya msingi kupiga pasi sahihi, kutengeneza nafasi na kuzuia vizuri.
Kali Ongala ni kama alishaisoma Simba na kufahamu anakwenda kukabiliana nayo vipi, kwanza alikubali kuwaachia mpira wakati ambao wanaanzisha mashumbulizi kwa kutengeneza nafasi na kuweza kuwakabia kwenye eneo la katikati huku katika eneo la kiungo, wachezaji zaidi ya wanne walikuwa wnakabiliana na viungo wawili wa Simba.
Ilikuwa ni rahisi kwa wachezaji wa Azam kwa sababu wachezaji wengi wa Simba hawakuwa tayari katika kukimbia, kuwania mipira na walikubali kupoteza mipira mingi kirahisi, kama unakosa ufanisi wa kupiga hata pasi ya mita thelathini hilo ni tatizo la mchezaji sio kocha, Azam walicheza mechi nyepesi ambayo walistahili kushinda.
Simba iliacha mianya mingi kwenye eneo lao wasipokuwa na mpira, eneo la kiungo namawinga wao wawili kukosa makali.





No comments:
Post a Comment