HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 19, 2013

DIAMOND AISAMBAZA VIDEO YA 'UKIMWONA’


Na Elizabeth John

MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’ ameisambaza video ya ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Ukimwona’ ambayo inafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, Diamond alisema kazi hiyo ameisambaza juzi katika vituo mbalimbali vya televisheni na kwamba anaamini itafanya vizuri kutokana na ubora wa mazingira aliyotumia kushuti video hiyo.

 “Najua mashabiki wangu wananijua vizuri sijaja kuuza sura mjini, naomba mashabiki wangu wakae mkao wa kula kwajili ya kuzipokea kazi zangu zingine zinazofuata kwani nina mashairi mengi yanasubiri muda tu wa kuingia mtaani,” alisema.

Diamond ni kati ya wasanii ambao wanafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya huku akitamba na baadhi ya ngoma zake kama Kesho, Mapenzi basi, Ritha na nyinginezo.

No comments:

Post a Comment

Pages