SIMBA MBENDEMBENDE KWA YANGA YACHAPWA 2-0

Beki wa Simba, Musa Mudde (kushoto) akichuana na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, leo. 
Beki wa Simba, Shamte Ramadhani akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Canavaro' akiwa amenyanyua kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara pamoja na wachezaji wenzake.
Shabiki wa Yanga akipelekwa kupewa huduma ya kwanza baada ya kuzimia wakati mchezo ukiendelea.
Kikosi cha Simba.
Makocha wa yanga wakipanga mikakati ya Ushindi.
Timu zikiingia uwanjani.
Timu zikisalimiana.
Kocha wa Simba, Patrick Liewig
Kocha wa Yanga, Ernst Brandts
Beki wa Simba, Shomari Kapombe akimtoka mshambuliji wa Yanga, Simon Msuva
Msanii Juma Nature akitumbuiza wakati wa mchezo huo. 
Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akitafuta mbinu za kuwatoka mabeki wa Yanga. 
Mashabiki wa Yanga.
 Raha ya ushindi.
 Kocha wa Yanga, Ernst Brandts akiwa amebebwa na wachezaji wake.
 Kiduku
KARIBU JANGWANI NGASA
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu yao. 
Mashabiki wa Yanga.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Simba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa  jijini Dar es Salaam
Kipa wa Simba, Juma Kaseja akijaribu bila mafanikio kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu katika mchezo wa kufunga pazia la Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
KARIBU NYUMBANI
Mashabiki wa Yanga wakiwa wamembeba mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngasa mara baada ya mpira kumalizika, ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika klabu yao. 
Refa wa mechi ya Simba na Yanga, Nartin Saanya akiwa chini baada ya kugongwa kwa bahati mbaya na mchezaji wa Yanga, Didier Kavumbagu.
Refa, Martin Saanya akipata matibabu.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Mheshimiwa Profesa Ibrahim Lipumba amekaririwa na Gazeti la Mwananchi la leo, Jumatano, Mei 15, 2013 akisema kuwa “amenasa taarifa za siri za kuwepo kwa mipango ya kuongeza muda wa Serikali ya sasa kukaa madarakani”.

Katika habari hiyo iliyoandikwa chini ya kichwa cha habari, “Lipumba: Kuna njama za kumwongezea JK muda” Mheshimiwa Lipumba anadai kuwa Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete “ itakaa madarakani hadi mwaka 2017”  kwa sababu kuna “wasiwasi kuwa mchakato wa sasa wa kupata Katiba Mpya hautaweza kukamilika mwaka 2014.”

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inapenda kufafanua kuwa taarifa hiyo ya Mheshimiwa Prof. Lipumba ni uzushi mtupu na ni upotoshaji usiokuwa na msingi.  Rais Kikwete hafahamu kuwepo mipango hiyo.  Ni vyema Mheshimiwa Lipumba aisaidie jamii kusema nani anafanya mpango huo ili ukweli ujulikane.  Aidha, Mheshimiwa Rais anawasihi wanasiasa na Watanzania kwa ujumla kuacha tabia za uongo na uzushi na kuwapotezea muda Watanzania kufikiria mambo yasiyokuwepo.

Ukweli ni kwamba, kama ambavyo amesema mara nyingi, ni matarajio ya Rais Kikwete kuwa mchakato wa Katiba utakamilika mwaka 2014 na kuwezesha Uchaguzi Mkuu wa 2015 kufanyika chini ya Katiba Mpya kama inavyotarajiwa na kumpa nafasi ya kustaafu mwisho wa kipindi chake cha uongozi wa taifa letu. 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
15 Mei, 2013

WANAKIJIJI WAMKATAA MWENYEKITI WAO

Na Bryceson Mathias, Morogoro

Wananchi wa Kijiji cha Makamba-Kidatu Mkoani Morogoro wamemkataa Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji chao, Ndenda Tidi na Halmashauri yake, ambapo tangu 10.3.2012 waligomea kufanya kazi za Maendeleo na Michango yoyote, hadi wasomewe mapato na matumizi ambayo hawajawahi kusomewa.

Wanakijiji hao walitoa dukuduku lao wakati wa mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wanakijiji hao walisema kuwa kiwanja cha Kliniki kimeuzwa kwa thamani ya sh. milioni 7 kwa mfanyabiashara mmoja.

Akihutubia Mkutano huo Mwanachama na Mwanaharati wa Mabadiliko ya M4Cwa CHADEMA Methew Likwina alisema, kama wananchi wa Mkamba wasipobadilika na kukataa kutumiwa kama vyombo vya Tija kwa Mafisadi, wataendelea kuwa watumwa kwenye nchi yao.

“Ni aibu kwa Viongozi wa Serikali ya Kijiji hiki, kuwadanganya wananchi kuwa wamekopa Shilingi laki 550,000/- kwa mfanyabiashara mmoja ili zisaidie maendeleo ya kijiji na kuwalazimisha wachange fedha ili kulipa, wakati ni Uongo kumbe Uongozi wa Kijiji unadaiwa urejeshe fedha za Kiwanja hicho.

”Chadema tunazo taarifa za mauzo ya Kiwanja cha Kliniki alichouziwa Mfanyabiashara mmoja hapa Kijijini (Nyaraka tunazo), ambapo baada ya CHADEMA kupiga kelele, Mwenyewe anataka arudishiwe fedha Zake! Wananchi hawawezi kulipa deni, Lipeni ninyi”.alisema.

Naye Mwenyekiti wa CHADEMA Kijijini humo, Lugano Mwambalaswa, alikiri kuwapokea wabachama hao 15 waliorudisha Kadi zao na kupewa Kadi mpya za Chama chake, ambapo waliahidi kutoa Ushirikiano Mkubwa ili kuharakisha Mabadiliko nchini Kote yanafanyika.

Diwani wa Kata ya Kidatu, Asajile Mwasumbi (CUF,) amekiri kuwepo kwa kosa la uuzaji wa Kiwanja hicho, ambacho anasema, tangu mwaka 1967 kiliashainidhwa kuwa pajengwa Kliniki, lakini Mwenyekiti Tidi (CCM) kwa uroho, aliuza na wananchi wamegomea kufanya kazi zote Maendeleo.

Aidha wananchi kwa upande wao, wamewatuhumu Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Hassan Masala, na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilombero, Azimina Mbilinyi, kuwa ndio wanaokwamisha maendeleo yao kwa kuwakumbatia waovu.

Katika mkutano huo Chadema kimevuna wanachama 15 kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa madai wamekasirishwa na Serikali yao ya Kijiji, kwa kuuza Kiwanja ch Kliniki kwa Milioni Saba.

Thamani ya Fedha Kenya 'Yawaachisha' Shule Wanafunzi Rombo

 Hizi ni baadhi ya njia zisizo rasmi kwenda nchini Kenya zilizopo eneo la Rongai, Rombo
 Sehemu ya Soko la Tarakea, Rombo. Soko hili ni miongoni mwa masoko yaliopo jirani na mpakani wa Kenya na Tanzania wilayani Rombo ambapo wananchi wa pande zote za mpaka huingia na kujipatia mahitaji yao kama wanavyoonekana.
Mkuu wa Sekondari ya Tanya, Victus Kiwango akizungumza na mwandishi wa www.thehabari.com hivi karibuni wilayani Rombo. 

Na Thehabari.com, Rombo

KUFANYA vizuri kwa thamani ya fedha ya Kenya (Kshs) tofauti na ile ya Tanzania (Tshs) kumechangia kwa namna moja kuiathiri Wilaya ya Rombo maeneo ya mpakani mwa Kenya na Tanzania kitaaluma kwa kile baadhi ya wanafunzi wa sekondari kuacha shule na kwenda kufanya vibarua vijiji vya jirani.

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni mjini hapa kumebaini kuwepo na idadi kubwa ya wanafunzi wa sekondari wa shule za mpakani wanaotoroka shule, ama wengine kuacha shule kuendelea na shule baada ya kumaliza elimu ya msingi hata kama wamefaulu na kwenda kufanya vibarua mpakani kwa kuvutiwa na thamani ya fedha ya Kenya.

Uchunguzi uliofanywa katika sekondari za Ngaleku, Tanya, Holili, Nduweni na Urauri zote zilizopo maeneo ya mpakani mwa Kenya wilayani Rombo umebaini idadi kubwa ya wanafunzi huzikimbia shule kabisa na wengine kufanya utoro wa rejareja wawapo shuleni kwa malengo ya kufanya vibarua mpakani.

Kwa shule ya Sekondari Urauri kati ya wanafunzi 238 waliopangiwa kujiunga na shule hiyo kwa mwaka huu ni wanafunzi 178 tu ndiyo walioripoti huku idadi kubwa ikidaiwa kukimbilia nchi jirani ya Kenya kufanya vibarua anuai zikiwemo kazi za ndani na mashambani kwa kuvutiwa na thamani ya fedha nchini humo.

Licha ya idadi hiyo kutojiunga na shule na kudaiwa kukimbilia Kenya, baadhi ya wanafunzi waliojiunga na shule nao huendelea na utoro wa rejareja hasa kipindi cha msimu wa kilimo, mavuno na palizi na kwenda kufanya vibarua hali ambayo huathiri maendeleo ya kitaaluma kwa shule na wanafunzi.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Holili, Benson Samizi alisema kati ya wanafunzi 140 waliofaulu na kupangiwa kujiunga na shule hiyo kwa mwaka huu ni wanafunzi 85 tu ndiyo walioripoti. Alifafanua kuwa 30 alipata taarifa waliamua kujiunga na shule nyingine huku idadi iliyobaki wakitokomea kusiko julika na shule inaendelea kuwatafuta.

Kwa upande wa Mkuu wa Sekondari ya Tanya, Victus Kiwango alibainisha kati ya wanafunzi 94 waliopangiwa kujiunga na shule hiyo kwa mwaka huu ni wanafunzi 79 tu ndiyo waliripoti shuleni. Aidha alisema utoro pia umeiathiri shule hiyo kitaaluma kwani matokeo ya kidato cha nne ya mwaka jana jumla ya wanafunzi 71 wamepata sifuri, hakukuwa na ufaulu wa daraja la kwanza wala la pili na wanafunzi wawili walipata daraja la tatu huku wanafunzi 18 wakipata daraja nne.

Mzazi mmoja aliyejitaja kwa jina la Protus Shirima alisema si wanafunzi pekee ambao huvutiwa na thamani kubwa ya fedha ya Kenya kwani hata wapo wazazi ambao hukimbilia kufanya vibarua Kenya vijiji vya mpakani kutokana na thamani ya fedha. Alisema kibaya zaidi wapo baadhi ya wazazi ambao huambatana na watoto wao katika vibarua hivyo ili kuongeza kipato cha familia.

"Mi nakushauri jaribu kuja msimu wa kilimo ukichanganya ukae eneo hili (Tarakea) utaona makundi makubwa ya wananchi wakivuka mpakani nyakati za asubuhi kuelekea Kenya kufanya vibarua na kurejea tena jioni...hali hii hufanyika vivyo hivyo wakati wa mavuno na palizi, fedha ya Kenya ipo juu na ndiyo inayotuvutia wengi," alisema Shirima.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Rombo, Judethadeus Mboya akizungumzia hali hiyo alikiri kuwepo na wimbi la wananchi kujiushisha na shughuli za mpakani maeneo hayo, japokuwa alisema wameanza utaratibu wa kuwatoza faini baadhi ya wazazi wanaoshindwa kuwazibiti watoto wao kiutoro shuleni kwa kuwatumia viongozi wa vijiji.

Aidha aliongeza kuwa ni vigumu kuwadhibiti wanafunzi kufanya shughuli za mipakani kwa kuwa wanapokwenda maeneo hayo hawaendi na sare za shule, ukiachilia mbali kuwa wapo baadhi ya wanavijiji wa Tanzania pia huendesha shughuli za kilimo nchini Kenya katika vijiji vya jirani.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com

WAJUMBE WA BODI YA UDHAMINI SSRA WALIPOTEMBELEA BANDA LA NSSF KATIKA MAONESHO YA WIKI YA HIFADHI YA JAMII MJINI DODOMA

Mjumbe wa bodi ya Wadhamini SSRA, Kabeho Solo akisaini kitabu cha wageni wakati wajumbe wa bodi hiyo walipotembelea banda la NSSF. Kulia ni Ofisa Mwandamizi Miradi na Uwekezaji, Gerlad Sondo na Ofisa Mwandamizi Uhusiano na Huduma kwa  Wateja, Theopista Muheta.
Ofisa Mwandamizi Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Theopista Muheta (kulia) akimkabidhi jarida lenye maelekezo ya kujiandaa kustaafu kwa mfanyakazi (staafu bila hofu), Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Irene Isaka  wakati wakati wa wajumbe wa bodi ya udhamini ya SSRA walipotembelea banda la NSSF kwenye maonesho ya Wiki ya Hifadhi ya Jamii inayoendelea mjini Dodoma. Katikati ni Ofisa Mwandamizi Miradi na Uwekezaji, Gerlad Sondo. (Na Mpiga Picha Wetu)
 Ofisa Uwekezaji na Miradi Mwandamizi wa NSSF, Gerald Sondo (kushoto) akitoa maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF katika maonesho ya Wiki ya Hifadhi ya Jamii.
 Wajumbe wa bodi ya Wadhamini SSRA wakitembelea banda la NSSF.
 Wajumbe wa Bodi ya Udhamini SSRA wakiwa katika banda la NSSF.
 Ofisa Uwekezaji na Miradi Mwandamizi wa NSSF, Gerald Sondo (kushoto) akitoa maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF katika maonesho ya Wiki ya Hifadhi ya Jamii.

Rais Kikwete aongoza Sherehe za maadhimisho ya mifuko ya jamii

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau na viongozi wa mifuko ya hifadhi ya jamii wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya Mifuko hifadhi ya ya jamii iliyofanyika mjini Dodoma leo. (Picha na Freddy Maro)

WENGI WAJITOKEZA WIKI YA HIFADHI YA JAMII

 Afisa Masoko na Elimu kwa Umma wa Mfuko wa Bima ya Afya, Grace Michael akimpa maelekezo juu ya shughuli za mfuko Mwenyekiti wa Bodi ya SSRA, Jayne Nyimbo
 Mmoja kati ya watu walihudhuria maonesho hayo akipatiwa huduma ya afya na afisa wa NHIF.
 AfisaMasokowa SSRA, Naima Bakari akitoa maelezo ya kazi Kuu za Mamlaka kwa wananchi wa Dodoma.
 Mmoja kati ya wananchiwa Dodoma akijiandikisha katika banda la SSRA
 Afisa Masoko wa SSRA, Naima Bakaria kitoa maelezo ya kazi kuu za Mamlaka kwa wananchi wa Dodoma
Mh Arden Rage akijiandikisha katika banda la GEPF baada ya kupata maelezo ya Mfuko kutoka  kwa, Aloyce Ntukamazina na Josephat Mshana
 Bw Lewis NgirwaakielezeafaidayakujiunganaMfukowa GEPF
 Afisa Uwekezaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF Bi. Anna Shayo akimkabidhi kitambulisho cha uanachama Mh. Margaret Agnes Mkanga, Mbunge wa Viti Maalum mara baada ya kujiunga na PPF alipotembelea banda la Mfuko.
Mbunge wa Viti Maalum Mbeya Mh. Dr. Mary Mwanjelwa  akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Mfuko wa PPF Kutoka kulia ni  Afisa Majanga wa Mfuko Bw. Noel Assenga, Meneja  Uhusiano Bi. Lulu Mengele na Mhasibu wa PPF  Bi. Grace Fihavango alipotembelea banda PPF.