Na Elizabeth John
MSANII wa muziki wa kizazi kipya
nchini, Said Juma ‘Chege Chigunda’ amesema ataendelea kufanya video za kazi
zake hapa nchini mpaka mashabiki waelewe anachokifanya katika tasnia hiyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam
jana, Chege alisema wasanii wengi hawathamini vya kwao na ndio maana wengi
wanaenda kufanya video nje ya nchi na kuacha studio za nyumbani.
“Hivi hatuwezi kuendelea hata
kidogo kama tunashindwa kuthamini vya kwetu hatuwezi kupiga hatua, hivyo
nawashauri wasanii wenzangu tuvikulai na kuvipenda vya kwetu,” alisema Chege
msanii kutoka kundi la Temeke Wanaume Family.
Chege kwasasa anatamba na ngoma yake ya 'Wauwe' ambayo inafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio kutoakana na maudhui ya wimbo wenyewe kuiteka jamii iliyomzunguka.
No comments:
Post a Comment