HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 25, 2014

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA), YAKITOZA FAINI KITUO CHA TELEVISHENI CHA CLOUDS NA RADIO CLOUDS FM KWA KUKIUKA MAUDHUI YA UTANGAZAJI


Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Margaret Munyagi (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Agosti 22, 2014 jijini Dar es Salaam, wakati akisoma maamuzi yaliyofikiwa na Mamlaka hiyo kuhusu shauri la ukiukaji wa kanuni za utangazaji namba 5/2014 dhidi ya Kituo cha Televisheni cha Clouds na Kituo cha Clouds Intertainment FM Radio cha Dar es Salaam. Kushoto ni Mjumbe wa Kamati hiyo, Bgoya Walter.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Margaret Munyagi (wa pili kulia), akiwa na wajumbe wenzake wakati wa mkutanmo huo. Kutoka kushoto ni Abdul Ngarawa, Joseph Mapunda, Walter Bgoya na Mkurugenzi wa Utangazaji (TCRA), Habby Gunze. (Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)


Wajumbe wa kamati hiyo, Abdul Ngarawa, Joseph Mapunda wakiwa kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Margaret Munyagi (kushoto), akitia saini maamuzi hayo kabla ya kupewa walengwa. Anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Utangazaji TCRA, Habby Gunze.
Wawakilishi kutoka Clouds Entertainment FM Radio wakiwa kwenye mkutano huo.
Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Pages