NA SULEIMAN MSUYA
BENKI
ya Amana na Kampuni ya Property International (PIL), zinewezesha
wateja zaidi ya 300 wa benki hiyo kumiliki viwanja venye hati miliki kwa
kipindi cha miaka mitatu.
Hayo
yamesemwa na Mkuu wa Idara ya Biashara wa Benki ya Amana Munir Rajab
wakati akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kuwakabidhi
hati wateja na kutangaza kuendelea na biashara ya umilikishaji viwanja
na PIL.
Rajab alisema
benki hiyo iliingia mkataba na PIL ambao uliwezesha wateja wa benki hiyo
kukopeshwa viwanja na kulipa kwa kipindi cha miaka mitatu ambapo
mafanikio yameonekana.
Mkuu
huyo wa Idara alisema utaratibu huo wa kuwawezesha wateja wao kumiliki
viwanja umekuwa na manufaa makubwa hivyo wamekubali kuongeza muda wa
mkataba.
"Amana benki
imedhamiria kubadilisha maisha ya Watanzania na moja ya njia ya kufikia
malengo hayo ni wananchi kumiliki viwanja vyao venye hati ili waweze
kupata mikopo itakayowasidia kuwekeza," alisema.
Rajab
alisema kuanzia sasa mteja wa benki hiyo ambaye atapata mkopo wa
kiwanja atatakiwa kurejesha baada ya miaka mitatu kutoka mmoja na nusu
wa awali.
Aidha, alisema wamewapunguzia faida kutoka asilimia 14 hadi 12 kwa mwaka ili waweze kurejesha kwa wakati.
"Mteja
anatakiwa kutanguliza asilimia 20 ya thamani ya kiwanja kama malipo ya
awali na kulipa kiasi kilichobaki kwa muda usiozidi miaka mitatu na kila
mita ya mraba moja atapata punguzo la shilingi 1,000, " alisema.
Mkuu
huyo wa Idara alisema watatumia wiki ya huduma kwa wateja inayoanza
Novemba 19/2018 hadi Novemba 24/2018 kuuza viwanja kwa bei ya punguzo.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Undeshaji wa PIL, George Obado alisema ubia
huo walioingia na Amana benki umekuwa mkombozi wa watanzania wengi.
Alisema
viwanja ambavyo vinauzwa na PIL vina ukubwa wa kuanzia mita za mraba
300 hadi 1,000 na kwamba miundombinu inazingatiwa katika kuvigawa.
Obado alitoa wito kwa wateja wa benki hiyo kutumia fursa hiyo ili waweze kujipatia viwanja vya bei rahisi na vyenye hati miliki.
Wanufaika
Nora Laizer, Aisha Spana na Stephen Mathias ambao ni wateja wa benki
hiyo walisema mkopo huo wa viwanja umewahakikishia maisha bora na
kuahidi kutumia hati hizo kukopa fedha iki wajikite katika
ujasiriliamali.


No comments:
Post a Comment