Makamu wa Rais wa Kampuni ya Mafuta ya Total Kanda ya Afrika, Kaskazini, Kati na Afrika Mashariki, Jean Philippe Torres (wa kwanza kulia), Rais wa Total Africa, Stanislas Mittelman (wa pili kulia), Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Total Tanzania,Tarik Moufaddal (wa tatu kulia), wakibadilishana mawazo na Mariane Saw, (wa kwanza kushoto), na Marsha Msuya Kileo, Mwanasheria na Mkurugenzi wa Uhusiano wa Total, wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Total Tanzania, jijini Dar es Salaam juzi. (Na Mpiga Picha Wetu).
NA SALUM MKANDEMBA
SERIKALI
ya Tanzania kwa kushirikiana na Kampuni ya Mafuta ya Total, itafanya utafiti wa
mafuta nchini, ambayo yakipatikana yataubadili uchumi wa Tanzania kwa kuongeza
kasi ya kuifanya nchi ya Uchumi wa Kati, kutegemeana na kiwango cha mafuta
kitakachogunduliwa.
Hayo
yamebainishwa na Waziri wa Nishati, Medard Kalemani, wakati wa hafla ya
kuwapongeza wafanyakazi na wadau wa Total Tanzania, katika Maadhimisho Total
Kutimiza Miaka 50 nchini Tanzania, yanayoadhimishwa kwa wiki nzima kwa shughuli
mbalimbali.
Sherehe
ya Jubilee ya Maadhimisho hayo imefanyika katika Hotel ya Hyatt Regency,
Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam, ambako imeelezwa kuwa kasi ya ukuaji wa
uchumi wa Tanzania itakuwa kubwa, utakaoibadili kabisa taswira ya Tanzania kiuchumi.
Waziri
Kalemani alisema utafiti umethibitisha kuwa, kila mahali ilipogunduliwa gesi
asili chini yake kuna mafuta, hivyo Serikali imeanza mazungumzo na Kampuni ya
Total Tanzania, ili kufanya utafiti wa mafuta, hivyo kuwataka Watanzania
kuipatia kila aina ya ushirikiano kampuni hiyo mshirika muhimu wa maendeleo.
Aliipongeza
Kampuni ya Total kwa kazi zake kubwa sita zinazozifanya nchini Tanzania,
ikiongozwa na kuuza mafuta yanayoongoza kwa ubora, vilanishi vyenye ubora wa
hali ya juu, ikiwa ni pamoja na kujenga bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda
hadi Tanga Tanzania.
Pia,
Waziri Kalemani alibainisha kuwa Total inasambaza nishati mbadala ya nishati
jua, inatoa ajira za kudumu na za muda kwa Watanzania wengi, na kubwa zaidi ni
kwa Total kuchangia huduma kwa jamii, yote hayo ukiyajumlisha, yanachangia
maendeleo ya taifa.
Kwa
upande wake, Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Total Tanzania, Bw. Tarik
Moufaddal, alisema katika kipindi cha miaka 50, Kapuni ya Total imefanya
makubwa Tanzania, kufikia kuwa ndio kampuni inayoongoza kwa wingi wa vituo vya kuuza
mafuta yanayoongoza kwa ubora na na vilanishi vyenye ubora.
Sherehe
za Maadhimisho hayo, zilizinduliwa wiki iliyopita na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim
Majaliwa, ambapo pamoja na mambo mengine, aliwakabidhi zawadi mbalimbali
wafanyakazi wa muda mrefu wa Total Tanzania na wadau wa kampuni hiyo.
Total
Tanzania ni kampuni ya mafuta ya petroli ambayo iliingia Tanzania mwaka1969,
ambako hadi sasa inatumia utaalamu wake katika kutoa huduma za kuaminika kwa
wateja wake kwa mfumo wa kadi maalum ‘Kadi ya Total’ kwa ajili ya ununuzi wa
mafuta na huduma mbalimbali magari katika vituo vya mafuta vya Total.
Kwa
mujibu wa Moufaddal, hayo yote yanafanyika katika kujitanua kibiashara kuelekea
kwenye matumizi ya nishati mbadala,na kwamba Total Tanzania kupitia mradi wake
wa Total Access to Solar (TATS Project), inasambaza taa za nishati jua
zinazoitwa AWANGO kwa jamii ya Watanzania.
No comments:
Post a Comment