HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 04, 2019

BUNGE LIKIPITISHA BAJETI YA TRILIONI 11.94 YA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020

 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akijibu hoja za wabunge wakati wa kuhitimishwa kwa hoja za Mapato na Matumizi ya shilingi trilioni 11.94 ya Wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020, Bungeni Jijini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akieleza kuhusu makusanyo ya kodi kuongezeka, wakati wa kuhitimisha hoja za wabunge kuhusu Mapato na Matumizi ya shilingi trilioni 11.94 ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020, Bungeni Jijini Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akijibu hoja za wabunge kuhusu Bajeti ya Wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020, Bungeni Jijini Dodoma.
 aadhi ya wabunge na Mawaziri wakimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) na Naibu wake Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), baada ya kupitishwa kwa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya shilingi trilioni 11.94 ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020, Bungeni Jijini Dodoma.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, (wa tano kushoto), akiwa na watumishi wengine wa Wizara hiyo, wakifuatilia mijadala ya wabunge kuhusu Bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020, Bungeni Jijini Dodoma, ambayo ilipitishwa kwa kishindo.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) (kushoto), akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, (wa pili kushoto), kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Benny Mwaipaja, Bungeni jijini Dodoma.
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi (Mb) (kulia), akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, baada ya Bunge kupitisha bajeti ya sh. trilioni 11.94 ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020, Bungeni Jijini Dodoma.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya  Fedha na Mipango Bw. Doto James (wa kwanza kulia), akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Khatibu Kazungu, Mhasibu Mkuu wa Serikali Bw. Francis Mwakapalila, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Amina Shaabani na viongozi mbalimbali wa Wizara wakifuatilia uwasilishwaji wa Bajeti ya Wizara iliyosomwa bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani), Jijini Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akipongezwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji baada ya  kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara hiyo nje ya ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akipongezwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Doto James baada ya  kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara hiyo nje ya ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango akipongezwa na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako baada ya  kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara hiyo nje ya ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya  Fedha na Mipango Bw. Doto James, akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti   Mhe. George Simbachawene, nje ya ukumbi wa Bunge baada ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara hiyo Jiijni Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (wanne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (wa pili kulia) pamoja na viongozi mbalimbali wa Wizara na Taasisi zilizo chini ya Wizara baada ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara hiyo Jijini Dodoma. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango).

No comments:

Post a Comment

Pages