HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 30, 2019

TOENI RISTI ZA MAUZO KUONDOA MIGOGORO –TRA

NA TIGANYA VINCENT

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa wito kwa wafanyabiashara kujenga tabia ya kutoa risti na kuweka kumbukumbu za mauzo wanayofanya kwa ajili ya kuwa na taarifa sahihi zitakazokazosaidia kuwa na makadirio yatakayo toa picha halisi ya kodi wanazotakiwa kulipa kwa mwaka.
Hatua itasaidia kuondoa mvutano kati ya wafanyabiashara na Maofisa  wa TRA wakati wa ukadiriaji wa Kodi ambazo watakiwa kulipa na kuiwezesha Serikali kupata Kodi inayotakiwa.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Meneja wa TRA Mkoa wa Tabora Thomas Masese wakati wa semina ya uelimishaji wafanyabiashara wa Wilaya mbalimbali za Mkoa huo.

Alisema baadhi ya wafanyabiashara wanapouza bidhaa kwa wateja hawatoi stakabadhi na wengine hawaweki kumbukumbu za mauzo ya kila siku jambo linalosababisha ugumu kwa Maofisa wa TRA kujua mauzo halisi.

Masese alisema wafanyabiashara wa aina hiyo wanapokadiriwa Kodi wanalalamika kuwa wanaonewa ,wakati wangekuwa wanatoa stakabadhi wasikuwa na mvutano na Maofisa wa TRA.

“ Ndugu ili kuondoa mvutano wakati wa ukadiriaji wa kodi  ni vema mkatoa risti na kuweka kumbukumbu za mauzo yenu ya kila siku…yatatusaidia kujua mauzo yako kwa mwaka na kodi ambayo mnapaswa kulipa” alisema.

Naye Afisa Elimu na Huduma kwa Mlipa Kodi wa TRA Mkoa wa Tabora Geofrey Comoro aliwataka wafanyabaishara ambao wamesajiliwa na kupewa Namba ya Mlipa Kodi (TIN namba) ambao biashara zao zimeyumba kuandika barua ili Maofisa wa TRA wafike kwao kuona hali halisi.
Alisema kitendo cha kutoa taarifa , TRA itaendelea kumuhesabu kama mfanyabiashara anayepaswa kulipa kodi kama ilivyokuwa siku za awali.

No comments:

Post a Comment

Pages