HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 30, 2019

MENEJA WA TRA MKOA WA TABORA KUWEKA KAMBI SIKONGE

NA TIGANYA VINCENT

MENEJA Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wa Tabora Thomas Masese amesema anatarajia kuweka kambi Wilayani Sikonge kutatua kero mbalimbali zinawakabili wafanyabiashara wakati wa ulipaji kodi.

Hatua inalenga kuondoa mvutano kati ya wafanyabiashara na watumishi wa TRA na kuongeza  makusanyo ya Serikali.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Meneja wa TRA Mkoa wa Tabora Thomas Masese wakati wa semina ya uelimishaji wafanyabiashara wa Wilayani Sikonge iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

Alisema anataka atumie muda mwingi wa kusikiliza kero na matatizo ya mfanyabiashara mmoja  baada ya mwingine ili kujua vikwazo mbalimbali vinavyowakabili kwa ajili kuleta mahuasiano mazuri yatakayosaidia  ukusanyaji wa mapato.

Masese alisema kutumia njia ya semina pekee hakuwezi kumaliza matatizo ya wafanyabiashara wote kwa sababu muda ni mfupi na wafanyabiashara wengi bado walitaka kueleza shida zinawakwaza wakati wa ulipaji kodi.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akifungua semina ya siku mmoja ya wafanyabiashara wa Sikonge aliwaonya Maofisa wa TRA ambao wanatumia lugha zisizofaa wakati wa utoaji wa huduma kwa wateja.

Alisema ni muhimu kujenga mahusiano mazuri ambayo yatasaidia ukusanyaji wa Kodi za Serikali kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo uboreshaji wa huduma za afya , maji na barabara.

No comments:

Post a Comment

Pages