HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 12, 2020

DC KISWAGA AIFAGILIA TIGO

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Festo Kiswaga, akikata utepe kuzindua duka la Tigo, lililopo Mtaa wa Sokoni wilayani humo. (Na Mpiga Picha Wetu).

 
NA MWANDISHI WETU, BARIADI

MKUU wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Festo Kiswaga ameyataka makampuni ya simu hapa nchini kuiga mfano wa Kampuni ya Simu ya Tigo ili kurahisha mawasiliano na huduma nyingine muhimu.
Kiswaga aliyasema hayo  leo wakati akizindua duka jipya la Tigo wilayani hapo ambapo aliyataka makampuni mengine kusambaa nchini kote ambavyo tigo imesambaa.
Alisema ufunguzi wa duka hilo utafungua fursa mbalimbali muhimu za kiuchumi na kuwaomba wananchi wa wilaya hiyo kulitumia kwa faida.
 “Tigo wanapaswa kupongezwa kwani wanafanya mambo makubwa na mazuri kwa wananchi hivyo ni jukumu la wadau wote wa mawasiliano kuangalia fursa hiyo kwa jicho la faida,” alisema.
Kiswaga alisema uwekezaji ambao umefanywa utaboresha huduma na kuhakikisha zinakidhi viwango vya kimataifa.
“Huduma bora kwa wateja ni kitovu cha biashara na zaidi huwafanya wateja wajisikie wanathaminika na kuheshimiwa, Tigo wametekeleza jambo hili kwa vitendo kwa kufanya uwekezaji katika utoajiwa huduma zao jambo linalowapa utofauti wa kipekee sokoni,” alisema.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka hilo, Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Uthmaan Madati alisema hatua ya kufungua duka hilo ni moja ya mkakati wa Tigo wa uboreshaji wa huduma na kuhakikisha zinawafikia wateja kwa wakati nchi nzima.
Alisema duka hilo litatoa huduma zote muhimu kuanzia usajili wa namba za simu kwa alama za vidole, huduma za kifedha ‘Tigo Pesa’ na mauzo ya data na vifaa vya mawasiliano kama simu janja, router na modem kwaajili ya huduma ya Tigo Home internet.
“Duka hili jipya litampa mteja wetu wasaa wa kutazama na kujaribu bidhaa mbalimbali kabla ya kuamua kufanya manunuzi.
Hatua hii imekuja kufuatia maombi ya muda mrefu kutoka kwa wateja wetu waliokuwa wakihitaji uwepo wa duka letu kwenye jengo hili maarufu kibiashara hivyo tumekidhi mahitaji yao,”alisema Madati.
Alisema duka hilo linakuwa la nne kufunguliwa mkoani humo huku likiwa na huduma mpya ikiwamo simu zinazotamba kwa sasa aina ya Kitochi 4G Smartpamoja na vifaa vya huduma za intaneti kwa makampuni maarufu kama ‘Tigo business’.

No comments:

Post a Comment

Pages