Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akizungumza katika uzinduzi wa huduma nne za Benki y UBA jijini Dar es Salaam.
Na Irene Mark
BENKI
ya UBA imezindua huduma nne mpya za akaunti maalum kwa ajili ya
kutimiza mahitaji ya kibenki ya wateja wake kulingana na umri na vipato
vyao.
Huduma hizo za akaunti pia zinalenga kurahisisha mahitaji ya wateja wa benki hiyo ya kifedha ya sasa na baadae.
Akaunti hizo ni UBA Malaika, UBA Janja, UBA Kizazi Kipya na UBA Hazina.
Mkuu
wa Kitengo cha Huduma za Rejareja Benki ya UBA, Geofrey Mtawa alisema
akaunti ya UBA Malaika inawalenga wazazi wanaotaka kuwawekea pesa watoto
wao kabla hajazaliwa hadi miaka 12.
Kuhusu
UBA Janja alisema ni maalumu kwa vijana wanaoanzia miaka 13 hadi 17
wakati UBA Kizazi Kipya ni kwa vijana walioanza kujiwekea akiba wakiwa
na miaka 18 hadi 25.
Kwa
mujibu wa Mtawa, UBA Hazina inawalenga vijana wa miaka 25 na kuendelea
kwa kuwa ni maalaum kwa ajili ya watu kwenye rika la kutaka kutimiza
ndoto zao, wanaojiwekea akiba ili kukidhi mahitaji yao ya shule, ujenzi
au biashara.
“Huduma
hizi ni utekelezaji wa malengo yetu ya kuwa benki kinara kwa kutoa
huduma bora za kibenki kwenye soko kwa kuzingatia maombi na mahitaji ya
wateja wetu, UBA tumeendelea kuvumbua huduma zinazorahisisha upatikanaji
wa fedha,” alisema Mtawa.
Hii sio mara ya kwanza UBA ikiongoza kwenye kuanzisha huduma bora za kibenki zenye kuleta mapinduzi yenye tija sokoni.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya UBA Tanzania, Usman Isiaka alisema benki yake
inalenga kurahisisha maisha ya kibenki na kuwapa wateja huduma bora
zenye ushindani mkubwa kwenye soko.
“Uanzishaji
wa huduma hizi unaendana na falsafa yetu ya UBA ya kumuweka mteja
mbele, ambapo benki inafanya vitu sio kwa jinsi inavyotaka bali kwa
jinsi wateja wetu wanavyotaka, muda wanaotaka na kwa njia wanayotaka
ziwe, ndio maana tukaangalia rika zote na kuhakikisha hatujamucha mtu
yeyote kuanzia mtoto akiwa tumboni, mwanafunzi wa shule, chuo,
wafanyakazi, wafanyibiashara na hata kizazi cha kuanzia miaka 25 na
kuendelea," alisisitiza Isiaka.
No comments:
Post a Comment