HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 12, 2020

TAASISI ZA MAFUNZO NA SEKTA YA UTALII ZAPEWA SOMO

NA FARAJA EZRA
NAIBU Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha, ameitaka Taasisi za mafunzo na wadau wa sekta ya Utalii  kufanya kazi kwa weledi pamoja ili kutatua changamto zilizopo ili kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2020.

Akizungumza na wadau hao jana jijini Dar es Salaam wakati wa kufunga Kongamano la Kimataifa la kuunganisha wanataaluma na wadau wa sekta ya Utalii na Ukarimu jijini humo.

Aidha alisema kumekuwepo na ushindani mkubwa katika soko hivi sasa  kutokana na  kuongezeka kwa wataalamu hao hivyo kunahitajika maandalizi mazuri ya rasilimali watu ili kuweza kushindana katika soko la dunia.

Waziri Ole Nasha alisema ya sekta ya Utalii ni moja ya Sekta inayolipatia Taifa fedha za kigeni kutokana na utalii hivyo alisema kukiwa na nguvu kazi yenye weledi na ufanisi wa kutosha nchi itaneemeka kupitia utalii.

“Hakika tunahitaji kuandaa vizuri rasilimali watu, nchi jirani zimepiga hatua kwenye kuvutia watalii sio kwamba wana vivutio vingi kuliko sisi ni kutokana na pamoja na mambo mengine kuwa na nguvu kazi yenye weledi ndio maana kama Taifa tunawekeza katika kutayarisha vijana ili kuwa na nguvu kazi yenye weledi katika sekta ya utalii,” alisema na kuongeza.

"Taifa letu linatoa kipaumbele katika kuimarisha viwanda ili kuleta mabadiliko ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuandaa nguvu kazi, hivyo ni vizuri kukawa na mfumo wa mafunzo pacha kati ya Taasisi za mafunzo na wamiliki wa viwanda", alisema Ole Nasha.


Hata hivyo ameipongeza chuo cha Taifa cha Utalii na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuandaa mkutano wa kuwaunganisha wakufunzi na watoe huduma hiyo walio katika biashara ya Utalii kwani kwa pamoja wanaweza kutatua changamoto zilizopo.

Naye Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Mlozi amewataka kuendeleza ushirikiano na vyuo vingine vinavyotoa mafunzo ya utalii ili  kuimarisha mpango wa utoaji mafunzo kwa kufanya kazi na watoa huduma ili kupata nguvu kazi yenye weledi na ujuzi kwa maslahi ya Taifa.

Alisema Soko la hotelia hivi sasa linapaswa kutoa nafasi kwa ajili ya walimu kupata ujuzi kwani kwa kufanya hivyo nchi itakuwa ya kwanza kuongoza kwenye sekta ya utalii na ukarimu nchini.
Pia Mlozi amesisitiza kuendeleza ushirikiano kati ya Taasisi hizo na wamiliki wa viwanda ili kuweza kutatua changamoto za ajira kwa vijana.

No comments:

Post a Comment

Pages