January 13, 2022

Achukua fomu kugombea uspika baada ya kuvutiwa na uongozi wa Rais Samia

 


Afisa  Mwandamizi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Doto Balele (kushoto), akikabidhiwa fomu ya kuomba kugombea nafasi ya Spika na  Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Oganizetion CCM Taifa, Solomon Itunda kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Halmashauri kuu ya Taifa (NEC),CCM Itikadi na Uenezi  Shaka Hamdu Shaka.



Na Asha Mwakyonde, Dodoma

AFISA Mwandamizi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Doto Balele amechukua fomu ya kuomba kugombea nafasi ya Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa  amevutiwa na uongozi wa Rais Samia Suluhu Hasaan kwa namna anavyoingoza nchi.

Akizungumza mara baada ya kukubidhiwa fomu hiyo leo jijini Dodoma Januari 13, 2022, na
Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Oganizetion CCM Taifa, Solomon Itunda kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Halmashauri kuu ya Taifa (NEC),CCM Itikadi na Uenezi  Shaka Hamdu Shaka endapo atapata nafasi ya kuwa Spika atakwenda kutatua changamoto mbalimbali  kwa wananchi.

Amesema uamuzi huo wa kuchukua fomu ni baada ya kuona wanawake wanaweza kushika nafasi za juu na kufanya vizuri  ambapo anatolea mfano kwa  Rais Samia ambaye anaongeza nchi.

Doto ameongeza kuwa Rais Samia amewapa mwamuko na kuwa tia nguvu wanawake kwa utendaji wake.

Afisa huyo Mwandamizi ameeleza kuwa  uwezo wa kuongoza Bunge anao na pia sifa za kugombea anazo kwa kuwa ni haki yake kugombea nafasi hiyo ya juu kwa mujibu wa katiba.

" Bunge linaongozwa kwa mujibu wa katiba na kanuni hivyo nitaenda kuzisimamia na kutakuwa na demokrasia bungeni endapo nitapata nafasi hii nitahakikisha natendea haki," amesema.

Pia amemshukuru Rais Samia kwa kazi nzuri anayofanya yenye maslahi ya Watanzania na kumuombea Mungu ampe afya njema.

No comments:

Post a Comment

Pages