Na Mwandishi Wetu
Klabu ya Yanga SC imetozea faini ya Sh. 5,000,000 (million tano) kwa kosa la kuingia chumba cha kuvalia kupitia mlango usio rasmi kuelekea mchezo dhidi ya Simba SC ulifanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam Oktoba 23, 2020.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania TPLB kutokana na kikao cha Kamati ya Uendeshaji na usimamizi wa Ligi kilichofanyika Oktoba 4. imebainisha kuwa.
"Adhabu hii ni kwa uzingativu wa kanuni ya 17:(21 na 60) ya Ligi Kuu kuhusu taratibu za mchezo." Imeeleza taarifa hiyo.
Ikumbukwe kuwa mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bao (1-1), Simba walijipatia bao kupitia kwa Agustin Okrah huku Yanga wakisawazisha kupitia kwa Stephan Aziz Ki.


No comments:
Post a Comment