HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 06, 2023

MKURUGENZI KIBAHA TC KUTOA MIKOPO YA MIL.700 KWA KINA MAMA

 


Katibu Tawala Wilaya ya Kibaha Sozi Ngate akinawa mikono mara baada ya kupanda mti aina ya mdodoma kwenye viwanja vya Halmashauri ya Kibaha ambapo amemwakilisha Mkuu wa Wilaya Kibaha Nickson John.




Na Khadija Kalili, Kibaha


MKURUGENZI wa Halmashauri ya Kibaha Mji Mhandisi Mshamu Munde ametoa ahadi ya kuongeza kiwango cha mikopo kwa wanawake na kina mama kutokana na jinsi walivyoonesha uaminifu wao katika  kurudisha mikopo yao kwa wakati.


Mhandisi Munde amesema hayo leo  Machi 6 katika  sherehe za maadhimisho siku  ya wanawake duniani  iliyofanyika   katika  Uwanja wa  Mailimoja  Soko la Zamani  iliyopo Kata ya Tangini Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.

 "Nawaahidi kina mama wote  watakao kidhi vigezo kuwa Halmashauri ya Mji Kibaha baada ya kujiridhisha  na kuwakagua kwenye ziara tulizo fanya na Idara ya Maendeleo tutawaongezea kiwango cha kukopa ili muweze kupaa zaidi kiuchumi.


Munde amesema kuwa "Tumeona  namna  ambavyo wanawake  wanavyo zalisha  bidhaa mbalimbali ambazo wamezizalisha kutokana na mikopo midogo tuliyowapa  awali pia nachukua fursa hiikuwapongeza  wanawake kwani  wanaongoza  katika kufanya biashara zinazoeleweka na wameonesha mioyo ya kujituma na wanaongoza kwa kurudisha mikopo hivyo sasa umefika wakati wa kuwaongezea kiwango cha fedha za kukopa     tutawakopesha kuanzia Mil.5 ,Mil.10 na kue delea" amesema Mhandisi Munde.

Akifafanua kuhusu kiwango cha fedha hizo Munde amesema kuwa Mil.400 nifedha zitakazopatikana kwenye mapato ya ndani huku Mil.300 ni fedha za marejesho ya mikopo waliyoitoa kwa kina mama wa Kibaha.


Sherehe hizo ziliambatana na shughuli za upandaji miti  katika eneo la Ofisi ya  Halmashaya Kibaha ambapo  Katibu Tawala  Kibaha Sozi Ngate ambaye alikua mgeni rasmi akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alipanda mti wa kumbukumbu na wengine waliopanda miti ni pamoja na Mhandisi Munde  , Afisa Mazingira Halmashauri ya Kibaha Ally Khatibu, Afisa  Maendeleo Hamlashauri ya Kibaha  Leah Lwanji.


Sherehe hizo zilipambwana  wahudhuriaji wakiwemo kikosi cha Askari wanawake kutoka Kambi ya Msangani Kibaha, wajasiriamali kutoka Kibaha , wafanyakazi kutoka Idara mbalimbali za Halmashauri ya Kibaha  na wakaazi wa wengine wa Kibaha.

No comments:

Post a Comment

Pages