HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 26, 2014

VIONGOZI WA UKAWA WAWASHA MOTO DAR

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia (kushoto) akiwaongoza wananchi kuimba wimbo wa Taifa  kabla ya kuanza kwa mkutano wa ushirikiano wa vyama vya siasa vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD. Kulia ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa Chadema, Freman Mbowe na Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba. (Picha zote na Francis Dande)
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Willbroad Slaa akihutubia katika mkutano wa Ukawa.
Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria mkutano huo.
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia akihutubia katika mkutano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika viwanja vya Jangwani.
Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba akitoa hotuba yake wakati wa mkutano wa Ukawa.
 Mwenyekiti wa Chadema, Freman Mbowe akihutubia katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chadema, Freema Mbowe akisalimia na Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Rajabu Katimba.
Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wakiingia kwa staili ya aina yake katika mkutano wa Ukawa.
Mwanasheria wa Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi (UKAWA), Tundu Lissu  akionyesha Katiba inayopendekezwa kwa wananchi ambayo wanaikataa.
Mwenyekiti wa NLD, Dk. Emmanuel Makaidi akitoa hotuba yake katika mkutano wa Ukawa.
Mfuasi wa Chama cha Wananchi CUF akiomba dua kabla ya kuanza kwa mkutano wa Ukawa.                     
Viongozi wa Ukawa wakitia saini hati ya ushirikiano wa vyama vya siasa vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD. Kutoka kushoto Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbati, Mwenyekiti Wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chadema, Freman Mbowe na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad. 
Umati wa watu waliohudhuria mkutano wa Ukawa.
Mwakilishi wa Mjimkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu akihutubia katika mkutano wa Ukawa.
 Umati wa watu waliohudhuria mkutano huo.
Viongozi wa Ukawa wakionyesha hati ya ushirikiano wa vyama vya siasa vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na NLD. Kutoka kushoto Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbati, Mwenyekiti Wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chadema, Freman Mbowe na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad. 
 Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba akiagana na wananchi waliohudhuria mkutano wa Ukawa.

No comments:

Post a Comment

Pages