HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 03, 2016

Bilioni 188.8 hupotea kutokana na vipimo vya Lumbesa

NA KENNETH NGELESI, MBEYA

JUMLA ya shilingi bilioni 188.8 zimekuwa zikipotea kila mwaka kutokana na vipimo vya Lumbesa kati ya hizo bilioni 14.8  serikali imekuwa ikipoteza kama mapato ya kodi huku wakulima nchini kote wakipata hasara ya zaidi ya sh Bilioni 174 kila mwaka.

Taarifa hiyo imetolewa na Dk. Goodluck Urassa wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Shule Kuu ya Biashara katika Mkutano wa wadau wa sekta ya biashara na kilimo katika Ukanda wa kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (SAGCOT) ulifanyika hivi karibuni jijini Mbeya kwa kushirikiana na taasisi zingine nyeti nchini vikiwemo baadhi ya vyuo Vikuu.

Akifafanua zaidi Dk. Urassa alisema tafiti zilizofanywa kwa kupitia mpango huo mwaka 2012 tulifanya utafiti wa vipimo vya mahindi na mpunga walibaini serikali na wakulima wenyewe wanapoteza fedha nyingi kwasababu ya ujazo huo wa ziada maarufu kama lumbesa.

Dk. Urassa alisema kutokana na hali hiyo wameanzisha mtandao utakao tafiti kero za kibiashara na kilimo katika mikoa hiyo na kuziwakilisha serikalini ili zifanyiwe kazi na kwamba serikali inakila sababu ya kuboresha mazingira ya biashara bna kilimo ili kutanue wigo wa ajira nchini.

Alisema kwa kupitia mpango huo ujulikanao kwa jina la (BEST) ambayo umelenga kuboresha mazingira ya biashara nchini utasaidia kuibua mambo mbalimbali yanayoongeza kero kwa wafanyabiashara na wakulima na kufanya utetezi.

“Tunashughulikia mambo ya kodi za mazao, vipimo, bidhaa feki, pembejeo feki. Tunafanya utafiti, tunatoa mafunzo na tunatoa ushauri na kufanya mazungumzo na serikali ili kuiboresha sekta hii ya biashara,” alisema Dk. Urassa

Alisema kuwa kuna utafiti mwingine unaoendelea kufanyika katika Mkoa wa Njombe juu ya matumizi ya pembejeo feki na athari ambazo serikali na wakulima wanapata ambapo  matokeo yake yatatolewa Februal mwaka.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtandao wa Multi Actors Integration (MAI), Lucas Mwakabungu alisema kuwa wadau hao kuwa ni pamoja na Chemba ya Wafanyabiashara, wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) ya mikoa ya Iringa, Morogoro, Mbeya, Njombe na Ruvuma ambayo yote ipo katika ukanda huo wa ujulikao kwa jina la (SAGCOT)

Katika hatua nyingine Mwakabunga alibainisha taasisi zingine zilizopo katika mtandao huo kuwa ni pamoja na Umoja wa Vyuo Vikuu Nchini, vyombo vya habari na washirika wengine katika sekta ya biashara na kilimo likiwemo Jukwaa la Wadau wa Kilimo Tanzania (ANSAF), taasisi inayojihusisha na kilimo cha mbogamboga, matunda na maua nchini (TAHA) na mpango wa SAGCOT wenyewe.

Alisema kwa kupitia ufadhili wa shirika la (BEST AC) mpango huo ni wa majaribio na umefanyiwa tafiti wa mwaka mmoja katika mikoa hiyo, na kwamba utafanywa pia katika mikoa mingine ili kuoanisha matokeo yake.

Mwakabungu alisema wadau hao watakaokutana mara mbili kwa mwaka wataongozwa na wawakilishi kutoka umoja wa vyuo vikuu kufanya utafiti huo na kutoa ushauri wa kuondoa vikwazo vya biashara serikalini ili iweze kuboresha mazingira mazuri ya biashara.

Mkutano huo ambao ulifanyika kwa muda wa siku mbili na jijini Mbeya ili kuainisha baadhi ya kero zinazoigusa sekta ya biashara na bada ya kuziainish,Kero hizo zitapelekwa katika vyuo vikuu ambavyo vimeshiriki zifanyiwe utafiti kabla ya kupelekwa serikalini kwa ajili ya kuzishughulikia.

Alizitaja baadhi ya kero hizo ambazo ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya biashara na wafanyabiashara wenyewe kuwa ni pamoja na wingi na ukubwa wa kodi na mikopo yenye riba kubwa.

Mwakabungu alisema utafiti wao wa awali unaonesha katika biashara moja nchini kuna kodi zaidi ya 20 huku wenye viwanda wakirundikiwa kodi zaidi ya 30 kwa mwaka jambo linalopunguza idadi ya walipa kodi badala ya kuongeza wigo wa walipa kodi.

No comments:

Post a Comment

Pages