HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 02, 2016

Deni la wafanyakazi Mtibwa lamkimbiza Meneja Mkuu, na Fedha kiwandani

Na Bryceson Mathias, Mvomero.

MENEJA wa Kiwanda cha Sukari Mtibwa, raia wa Afrika kusini, Greg Swart, na Meneja wa Fedha, wamewakimbia wafanyakazi wa Kiwanda hicho wanaodai Mshahara wa Mwezi Januari, baada ya Kufunga Milango yote ya kiwandani hapo.

Awali Uongozi wa Kiwanda hicho, ulitangaza kwenye Mbao za Matangazo kwamba, Mshahara huo utalipwa, Februari 13, jambo ambalo wafanyakazi hawakukubaliana kwa tarehe hizo wanatakiwa kulipwa Mshahara wa Kati (half payment).

Kutokana na sintofahamu hiyo, Diwani wa Kata ya Mtibwa, Luka Mwakambaya (Chadema), amewasiliana na Mkuu wa Wilaya, Betty Mkwasa, ili aende akawatatulie tatizo hilo Sugu (amekubali), ambalo wafanyakazi na wananchi wa eneo hilo wanaliita Donda Ndugu.

Kinachowatesa Wafanyakazi na Wananchi wa Kata ya Mtibwa, Meneja Swart, amekuwa Mwiba wa Uchungu kwao, kabla na baada ya kurejea tangu alipofukuzwa na Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, Septemba 7, 2010, kwa kutumia lugha chafu za matusi na za kudhalilisha wananchi, hasa waajiriwa.

Akiwa Kiwanda cha Sukari Mtibwa, na Wazee wa Mji Mdogo wa Madizini, Septemba 7, 2010, Kikwete alimwagiza aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Fatma Mwasa, sasa Mkuu wa Mkoa Geita, kukutana na makundi yanayohusika yakiwemo ya menejimenti na ya wakulima wa miwa.

Kufukuzwa kazi nchini kwa Meneja huyo raia wa Afrika Kusini, kulitokea baada ya Raisi  Kikwete kufika Mtibwa, Turiani wilayani Mvomero mkoani Morogoro, akiwa katika mikutano yake ya kampeni, ambapo alielezwa na Wananchi kero na matatizo yanayowakabili dhidi ya uongozi wa Kiwanda hicho.

Wakati wananchi wakiwa hawajaridhishwa na kurejeshwa kwake kinyemela, bado mioyo yao imeanguka kutokana na kuona, licha ya Mneja huyo kurejea kinyemela, bado hajajifunza na kujirekebisha makosa ya awali, na wanaishangaa Uhamiaji Meneja huyo kuwepo nchini.

No comments:

Post a Comment

Pages