HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 12, 2016

WAENDELEZAJI MILKI WAHIMIZWA KUFUATA SHERIA

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akizungumza katika Mkutano wa Wadau wa Uendelezaji Milki uliofanyika jijini leo Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula akifungua Mkutano wa Wadau wa Uendelezaji Milki uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Washika dau.
Wakifuatilia mkutano huo.
Wadau wakiwa katika mkutano huo.

NA MWANDISHI WETU

SERIKALI imewataka waendelezaji milki kote nchini kuzingatia sheria wanapokuwa katika ujenzi wa majengo mbalimbali.

Hayo yalielezwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Mabula, alipokuwa akifungua mkutano wa wadau wa uendelezaji milki uliofanyika Julai 12, mwaka huu, makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa, jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri huyo aliwakumbusha wajumbe wa mkutano huo kuwa waendelezaji milki wengi hapa nchini wamekuwa wakifanya shughuli zao bila kuzingatia sheria, hususan Sheria ya Ardhi Sura ya 13; Sheria ya Mipango Miji Na. 8 ya mwaka 2007 pamoja na Sheria ya Umilki wa Sehenmu ya Jengo Na. 16 ya mwaka 2008, hivyo kuwataka kila mmoja kuziheshimu.

“Wengine hubadili matumizi au kujenga majengo  marefu zaidi ya kiwango kilichoidhinishwa kwenye vibali  vya ujenzi bila idhini ya mamlaka husika. Pia wapo ambao hutumia vifaa duni vya ujenzi au hupunguza viwango kwa makusudi kwa lengo la kujiongezea faida na hatimaye husababisha maafa.  Hali Hii pia  husababisha migogoro na hasara ambazo zingeweza kuepukika. Aidha, husababisha miji mingi kuendelezwa  katika hali isiyopendeza,” alitahadharisha Angela.

 Naibu waziri huyo alizitaka halmashauri na mamlaka zote za usimamizi wa waendelezaji milki hapa nchini kuhakikisha zinatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria na taratibu  zilizowekwa.

Aidha, alizihimiza mamlaka hizo kuongeza kasi ya usimamizi na utekelezaji wa  miundiombinu na kuzitaka halmashauri kutoa hatimilki za ardhi na vibali  vya ujenzi kwa wakati bila kusahau jukumu lao la kusimamia na kukagua utekelezaji wa miradi ya ujenzi.

Vilevile aliwapongeza  wajumbe  hao kwa nia yao ya kuanzisha umoja ili kuwa  na sauti moja na yenye nguvu, kwa kuanzisha chama ambacho kitatambulika kisheria, ambacho kitawakilisha na kutetea masilahi yao, kusimamia maadili yao na kushawishi wanachama  kuzingatia sheria na kushindana kibiashara ndani ya   misingi ya ushindani ulio sawa.

No comments:

Post a Comment

Pages