HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 12, 2016

BENKI YA CRDB YAKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA 'SHINDA NA TEMBOCARD', SHAFFIH DAUDA AIBUKA MSHINDI

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akimakabidhi zawadi ya Laptop Macbook air, Shaffih Dauda baada ya kuibuka mshindi katika Shindano la 'Shinda na TemboCard'

NA IRENE MARK

MWANDISHI na Mchambuzi wa masuala ya soka hapa nchini, Shaffih Dauda ameibuka kidedea katika shindano la Shinda na Tembokadi linaloendeshwa na Benki ya CRDB.

Dauda ni miongoni mwa washindi wanne wa Julai ambao ni wateja wa benki hiyo waliotumia zaidi kadi zao katika kufanya manunuzi ya bidhaa mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuwatangaza washindi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk. Charles Kimei shindano hilo limehamasisha matumizi ya tembokadi za benki hiyo.

Dk. Kimei aliwataja washindi ambao ni wateja wa benki hiyo kwa Julai kuwa ni Nasir Mnkande aliyepata tiketi ya ndege kwenda Dubai pamoja na familia yake, Dauda aliyeshinda Laptop Macbook air.

Aliwataja washindi wengine ambao ni mawakala wa Fahari Huduma kuwa ni Benrad Swai aliyepata Laptop Mackbook Air na kampuni ya Mzenzi Investment iliyopata Ipad air.

“Tunalenga kuwavutia wateja wetu wengi zaidi ili waamini kwamba kufanya malipo kwa tembokadi ni rahisi, nafuu na salama… mteja habebi fedha nyingi ni kadi yake na namba ya siri tu.

“Mshindi ni yule atakayekuwa amefanya mihamala mingi yaani amenunua bidhaa mbalimbali kwa kuchanja kadi yake kwenye mashine za wauza bidhaa au huduma au kwa mwezi husika,” alisema Dk. Kimei ambaye ni mtaalam wa shughuli za kibenki kimataifa.

Alisema shindano hilo la miezi sita limeongeza mahitaji ya tembokadi hadi kufikia kadi milioni 1.6 na kusambaza vifaa vya manunuzi 1,500 kwa biashara na taasisi mbalimbali hapa nchini.

Hata hivyo walizawadiwa pia washindi wa Juni ambao ni Wakwetu General Supply na Deograsy Mlay walionyakulia Laptop Mackbook air, Eunice Manamba aliyepata Ipad air na Hassa Nyimbile aliyepata tiketi ya ndege kwenda Dubai na familia yake.

Shindano hilo linaendelea huku wateja wa CRDB wakimasishwa kushiriki kwa kutumia Tembokadi zao wanapofanya manunuzi ya gharama yoyote.

No comments:

Post a Comment

Pages