HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 12, 2016

Wamiliki shule watakiwa kutoa fursa kwa wakuu wa shule kupata mafunzo ya kitaaluma na uongozi

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania  (TEA), Joel Laurent, akizungumza na Wamiliki wa Shule na Vyuo visivyo vya serikali (TAMONGSCO) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Nyasa katika mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa JKT jijjini Mbeya. Kulia ni Mwenyekiti Tamongsco Taifa, Kitururu Mzava na Mwenyekiti Kanda, Asanga Ndile. (Picha na Kenneth Ngelesi)


NA KENNETH NGELESI, MBEYA

WAMILIKI na mameja wa shule zisizo za Serikali hapa nchini TAMONGSCO wameshauriwa kuwapeleka wakuu wa shule kushiriki semina na vikao mbalimbali vinavyo husiana na masuala ya kitaalumu badala ya gharama za kumsafirisha walimu kmushiriki vikao hivyo.

Wito huo ulitolewa jana na Mwenyekiti wa Wamiliki na Maneja wa Vyuo na shule zisizo za  Serikali TAMONGSCO,kanda ya nyanda za juu kusini Asanga Ndile baada ya kuona kuna idadi ndogo ya walimu wakuu na wakuu wa shule ikilinganishwa na wamiliki na mameneja wa shule katika kikao.

Akizungumza katika kikao cha dharura kilichofanyika juzi katika Bwalo la JKT katika Viwanja vya Nane nane Ndile alisema kuwa kumekuwa na tabia ya wamiliki wa shule kuto waruhusu walimu wakuu na wakuu shule na Vyuo, kushiriki vikao vya jumhiya hiyo kwani wao ndiyo wanajukumu kubwa na kuinua kiwanngo cha elimu katika shule zao badala ya wao na mameja wa shule ambao wengi wao hawana utaalamu katika masuala ya elimu.

‘ Hili nimeona katika kikao cha leo lakini pia hata kiliocho pita walioshiriki ni wachache sana,na tulicho kiona wengi hawana taaluma ya ualimu sasa umuhimu wa elimu hajui kuwa mwali8mu anatakiwa atumike zaidi sasa yeye anawaza nimsafirishe huyu hawezi kurudi na pesa kumbe kule atarudi na utaalamu uliondaliwa na tamongsco’ alisema

Alisema ushiriki wa wawakuu wa shule katika semina,Mikutano na warsha hizo watarudi na utalaamu wenye manufaa kwa ajili ya shule zao hivyo wanapaswa kuona umuhimu wa kutuma wakuu wa shule kuudhuria vikao, semina na mikutano hasa zile zinahusiana na masula ya kitaaluma.

Aidha Ndile alisema kuwa hivi sasa wapo katika ushindani wa kutoa elimu bora hivyo ili kukabiliana na hilo wanachama wake hawabudi kuwawwezesha wakuu wa shule kwani bila hivyo shule walizojenga yatabaki magofu.

‘Ndugu zangu tupo katika Ushindani kwanza sisi wenyewe lakini pia kuna ushindani na shule za Serikali hivyo hanabudi kuwawezesha walimu wetu wakuu kitaalumu hasa kushiriki Semina na Mikutano kama hii kwani wao ndiyo wataalumu na kuziwesha shule zetu kuendelea kufanya vizuri’ aliongeza Ndile

Kwa upande wake Mwenyuerkiti wa Jumuhiya hiyo taifa Kitururu Mzava alisema wakati wa kulala kwa wanachama wake umepita kwani sera ya elimu bure ni changamoto kwao.

Alisema kuwa hivi sasa Serikali imeanza kuboresha shule zake hivyo ni wakati mwafaka kwa wamiliki binafsi kuamka na kufanya vizuri zaidi ili ziendelea kuwa kufanya vizuri zaidi.

No comments:

Post a Comment

Pages