HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 06, 2018

TIMU YA WANAWAKE YA KLABU YA GOFU YA LUGALO YAAGWA LEO

 Mkuu wa  Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo  akimkabidhi Bendera  ya Taifa Nahodha wa Timu ya Wanawake ya Klabu ya Gofu ya Jeshi la Ulinzi la  Wananchi wa Tanzania ya Lugalo inayotarajia kushiriki mashindano ya Wazi ya Wanawake ya IBB  nchini Nigeria Hivi karibuni ( Picha na Luteni Selemani Semunyu).
 Mkuu wa  Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo  akisalimiana na Wachezaji wa Timu ya Wanawake ya Klabu ya Gofu ya jeshi la ulinzi la  Wananchi wa Tanzania ya Lugalo inayotarajia kushiriki mashindano ya Wazi ya Wanawake ya IBB  nchini Nigeria hivi karibuni. (Picha na Luteni Selemani Semunyu).
 Mwenyekiti wa wa Chama cha Gofu nchini Joseph tango (aliyesimama) akizungumza wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari  Makao Makuu ya Jeshi Upanga ambapo timu ya Wanawake ya Klabu ya Jeshi ya Lugalo walikabidhidhwa bendera kwa ajili ya kushiriki Michuano ya Wazi nchini Nigeria aliyeka Kushoto ni Mwenyekii wa  Lugalo Brigedia Jenerali Michael Luwongo Mstaafu. ( Picha na Luteni Selemani Semunyu).
Mkuu wa  Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo  akisalimiana na Afisa habari wa Klabu ya  Gofu ya Jeshi ya Lugalo  Luteni selemani Semunyu (kulia), baada ya kukabidhi Bendera  kwa Nahodha wa Timu ya Wanawake ya Klabu ya Gofu ya jeshi la ulinzi la  Wananchi wa tanzania ya Lugalo inayotarajia kushiriki mashindano ya Wazi ya Wanawake ya IBB  nchini Nigeria Hivi karibuni ( Picha na Luteni Selemani Semunyu).

 Na Luteni Selemani Semunyu JWTZ

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo amewataka wachezaji wa Timu ya Wanawake ya Gofu ya Klabu ya Jeshi ya Lugalo kuhakikisha wanarejesha heshma ya jeshi kuwa kinara katika michezo na kuzalisha wachezaji bora wanaowakilisha nchi  kwa mafaniko.

Aliyasema hayo Makao Makuu ya jeshi Upanga  Jijini Dar es Salaam  wakati akiagana na wachezaji Sita wa Gofu wanaotarajia kuwakilisha nchi katika michuano ya wazi ya wanawake nchini  Nigeria IBB Ladies Open Championship  2018 yanayaotarajia kufanyika hivi karibuni.

Jenerali Mabeyo alisema kama ilivyokuwa katika Michezo ya Riadha na Ngumi sasa tunataka na kwenye gofu na kwa kuanza ni timu hii ya Gofu ya Wanawake kuhakikisha inarudi na ushindi mnono.

“ Nikiwa mlezi wa Klabu naamini mtatuwakilisha vyema na Jeshi kwa ujumla tutaendelea kuwaunga mkono wachezaji  wa Gofu na hata Michezo mingine kuhakikisha jeshi linaendelea kuwa kinara w michezo nchini na kuwa chachu kwa wengine” Alisema  Jenerali Mabeyo.

Aliongeza kuwa licha ya matumaini yake katika Gofu lakini pia katika Soka licha ya Mchezo huo kutawaliwa na simba na yanga lakini sasa walau mwanga unaonekana baada ya ya Timu ya Jeshi ya Green Worriorrs kuifurusha Timu ya Simba katika Michuano ya Kombe la Shirirkisho.

“Ushindi ule ulikuwa Mwanzo mzuri wa kupunguza Ubabe wa Simba na Yanga na Ushabiki wa Simba na Yanga hata miongoni mwa Wachezaji hivyo nanyi kama mlivyofanya vyema katika mashindano Uganda sasa tunatarajia Ushindi toka Nigeria” Alisema  Jenerali Mabeyo.

Kwa Upande wa mwenyekiti wa Klabu hiyo Brigedia Jenerali Michael Luwongo  Mstaafu aliwataja wachezaji hao kuwa ni Nahodha Ayne Magombe, Sara Denis , Sophia Mathius ,Hawa Wanyenche ,Christina Charles  na Angel Eaton huku mkuu wa Msafara akiwa ni Kapten Japhet Masai. 

“ Nina matumaini makubwa na Kikosi hiki tunachokituma Nigeria naamini kitarejesha furaha kwa Klabu ,jeshi na Watanzania kwa ujumla ukizingatia uwezo Binafsi wa Wachezaji Mazoezi na Historia kutokana na michuano iliyotangulia” Alisema Brigedia Jenerali Mstaafu Luwongo.

Kwa Upande wake mwenyekiti wa Chama cha Gofu nchini TGU Joseph tango amelipongeza jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania kwa jitihada katika kuendeleza michezo hasa mchezo wa gofu ambao klabu ya Lugalo imekuwa kielelezo.

Aliomba mkuu wa majeshi ya ulinzi na Mlezi wa Klabu ya Lugalo kuendelea kuisaidia Klabu hiyo ambayo ndio klabu yenye mashindano mengi kwa mwaka ukilinganisha na Klabu nyingine nchini ikiwemo kusaidia utekelezaji wa Ujenzi wa Uwanja makao makuu ya nchi Dodoma.

Mashindano hayo ya Siku Tatu yanatarajiwa kuanza Tarehe Nane  Februari huku wachezaji kutoka nchi mbalimbali ikiwemo  Kenya,Uganda,  Zambia   na Malawi wakitarajiwa kushiriki.

No comments:

Post a Comment

Pages