HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 20, 2018

Mshindi wa Milioni 300 za Supa Mzuka Cup 2018 akabidhiwa Zawadi yake


Mkurugenzi wa mawasiliano wa TatuMzuka Sebastian Maganga akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani),wakati wa akimtambulisha
Mshindi wa kampeini ya ‘SupaMzuka Cup’ aliyeshinda katika fainali tarehe 15 Julai 2018 kitita cha milioni 300 za kitanzania,Abeid Amri mkazi kutoka Mbagala

Abeid Amri, 28 anayeishi Mbagala Wilaya ya Temeke Dar es Salaam ndiye ameibuka mshindi wa Jackpot kubwa kuwahi kutokea nchini Tanzania. Amri hakushinda peke yake bali alichagua timu yake ya watu 10 ili kukamilisha timu yake ya watu 11 ambapo kila mmoja amepata milioni 1. Mwakilishi kutoka kampuni ya michezo ya kubahatisha Abdallah Hemed
Wanahabari wakifuatilia tukio hilo
Mkurugenzi wa mawasiliano wa TatuMzuka Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi Mshindi wa kampeini ya ‘SupaMzuka Cup’ aliyeshinda katika fainali tarehe 15 Julai 2018 kitita cha milioni 300 za kitanzania,Abeid Amri mkazi kutoka Mbagala

TatuMzuka, mchezo wa namba unaoongoza nchini Tanzania leo umemkabidhi Mshindi wa kampeini ya ‘SupaMzuka Cup’ aliyeshinda katika fainali tarehe 15 Julai 2018 kitita cha milioni 300 za kitanzania.

Abeid Amri, 28 anayeishi Mbagala Wilaya ya Temeke Dar es Salaam ndiye ameibuka mshindi wa Jackpot kubwa kuwahi kutokea nchini Tanzania. Amri hakushinda peke yake bali alichagua timu yake ya watu 10 ili kukamilisha timu yake ya watu 11 ambapo kila mmoja amepata milioni 1.

“Tumepata faraja kubwa kushuhudia Mtanzania mwenzetu akipata ushindi mkubwa kiasi hiki. Umetuandikia historia leo kwa sababu haijawahi kutokea nchini Tanzania mtu kushinda million 300. ” Alisema Bwana Sebastian Maganga, Mkurugenzi wa mawasiliano wa TatuMzuka

Kwa Msimu huu wa SupaMzuka Jackpot watu wamecheza na kushinda na marafiki, na Bwana Amri pia alichagua timu yake ambao ni; 1 Mwanaidi Omary, 2.Subira Issa 3. Jasmin Issa 4. Shufwaa Issa 5. Farhat Issa 6. Omary Issa, 7. Amin Issa 8. Mwanaasha Omary, 9. Agness Samwel, 10. Magdalena.

“Mimi sijala vizuri, wala kulala tangu siku hiyo jumapili. Kila saa nawaza kama ni ndoto alafu nitaamka, lakini sasa naamini kabisa kwamba ni kweli nimeshinda” aliezea Amri. “Nina furaha sana na pia kushinda na marafiki, najiskia kama wengi tumeshinda!” alisisitiza Amri.

TatuMzuka imeuutarifu umma kwamba mshindi tiyari ameanza kupatiwa mafunzo kuhusu mikakati na mbinu za kutumia na kutunza fedha zake.“ Tangu alipopata Ushindi wake, tumeanza kumsaidia kutafuta wataalamu wa masuala ya utunzaji na uwekezaji wa fedha ili wawawe kumshauri namna nzuri ya kuwekeza fedha zake ili ziweze kumsaidia zaidi” alifafanua Bwana Maganga

TatuMzuka wanaendelea kuwapa watanzania fursa ya kuwa mamilionea . Kucheza Tatu Mzuka kupitia; MPESA, TIGO PESA na AIRTEL MONEY, unaingiza namba ya kampuni ambayo ni 555111 na baada ya hapo ingiza namba zako 3 za bahati kisha ingiza salio kuanzia shilingi 500 mpaka 30,000. Unaweza kushinda kila baada ya dakika 10, kila siku million 10 na Jumapili hii kuna Milioni 60.

No comments:

Post a Comment

Pages