HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 06, 2019

Muuza Matunda Zanzibar ashinda Jackpot Bonasi ya SportPesa Mil.6.8

 Na Mwandishi Wetu
MATESO Modesti (35^) wa Zanzibar ameibuka mshindi wa Bonasi ya Jackpoti kutoka SportPesa mara baada ya kushinda kwa usahihi ubashiri wake wa mechi 11 kati ya 13 ambazo amebashiri na kushinda shilingi 6,835,003
Modesti ni mfanyabiashara wa matunda huko Visiwani Zanzibar maeneo ya Darajani ambaye mara nyingi amekuwa akicheza michezo ya ubashiri SportPesa bila ya mafanikio ya kushinda kabla ya juzi kushinda.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Modesti alisema kuwa “Nilianza kucheza SportPesa, mwaka jana na ninashukuru kufanikiwa kushinda mwaka huu, kiukweli ilikuwa ndoto yangu kushinda siku moja bonsai hii, hivyo ninajisikia furaha.
“Baada ya ushindi huu wa bonasi, nimepanga kuiboresha biashara yangu ya matunda, mimi mfanyabiashara wa matunda  baada ya kufanikiwa kushinda ubashiri wangu kupitia Kampuni ya SportPesa inayoendeleshwa michezo hiyo ya ubashiri.
“Nilishinda ubashiri huu baada ya kushinda mechi 11 kati ya 13 ambazo zimewekwa na SportPesa,, hivyo nimepanga kuendelea kubashiri zaidi kupitia SportPesa hasa kwenye bonasi hii. 
 “Na nitacheza zaidi Jackopti bonasi kutokana na kiwango kikubwa cha fedha kilichowekwa ambacho ni kingi na uzuri wake ukishinda mechi zako, basi haraka unatumiwa ujumbe kuwa umeshinda bonasi na fedha unapatiwa.

“Hivyo siyo kampuni ya kijanjakijanja kama zilivyokuwa kampuni nyingine za kubet, hivyo nawashauri vijana wenzangu na wazee kucheza kupitia SportPesa,”alisema Modesti aliyepanga kuboresha biashara ya matunda kupitia biashara hiyo.

Meneja Uhusiano wa SportPesa Bi. Sabrina Msuya alimpongeza mshindi wa bonasi kwa ushindi wake na kumshauri pesa alizoshinda awekeze ili aweze kukuza biashara yake ya matunda na kujiongezea mtaji.

“Wiki hii JackPoti yetu imesimamia zaidi ya milioni 494,275,700/- ambapo inakaribia kufika nusu bilioni na tunatarajia kupata mshindi. Mteja anapaswa kuweka ubashiri wake kwa usahihi wa mechi 13 ili kujishindia kiasi hicho mbali na hapo bonasi hutolewa kwa watakaopatia mechi kuanzia 10-12.

No comments:

Post a Comment

Pages