HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 06, 2019

Mtaka awalipa wanariadha madeni yao

WAKATI Tanzania ikielekea kwenye maandalizi ya mbio za dunia za nyika mwaka huu, Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka amefanikiwa kutimiza ahadi ya kuwalipa wanariadha wote waliokuwa wana madeni yao kwa shirikisho hilo.
Wanariadha waliolipwa ni pamoja na wasichana  sita waliofanya vizuri kwenye mbio za Dunia za Nyika mwaka 2017 nchini Uganda kiasi cha shilingi milioni 4.8 kwa mgawo wa shilingi laki nane (800,000) kila mmoja fedha zilizokuwa zimetolewa na shirikisho la riadha la dunia (IAAF).
Wanariadha hao ni pamoja na Failuna Abdi Matanga, Anjelina Daniel Tsere, Magdalena Shauri, Sara Ramadhani, Mayselina Mbua, Siata Kalinga ambao waliibuka washindi wa sita kwa upande wa timu na kuifanya Tanzania kuzawadiwa kiadi cha dola 6000.
Wengine waliolipwa fedha zao ni wanariadha watatu wa Mbio za dodoma Marathon mwaka 2016, ambao walikuwa wazawadiwe mabati lakini zilipotea chini ya mikono ya uongozi wa RT.
Wanariadha Gabriel Geay (kwa upande wa wanaume) na Fadhila Salum (Kwa upande wa wanawake) waliokuwa washindi wa pili katika mbio zile alitakiwa kulipwa bati 100 kila mmoja ambapo walifidiwa kiasi cha shilingi milioni moja kila mmoja (1,000,000) huku  Catherine Lange aliyeshika namba tatu alikuwa anadai bati 40  alipatiwa kiasi cha shilingi 400,000.
 “Katika kuelekea mashindano mapya ya kimataifa, yaliyoko kwenye kalenda ya Shirikisho tumeona tulipe kwanza madeni yote ya wanariadha waliokuwa wanadai maana naona yanaleta maneno maneno mengi na yanaweza kuwa sio mazuri kwa afya ya mchezo wa riadha,” alisema Mtaka
Akitoa sababu za wanariadha kucheleweshewa fedha hizo, Mtaka alisema kuwa fedha hizo ziliingizwa na Shirikisho la Riadha Duniani (IAAF) kwenye akaunti isiyo sahihi ya RT, hivyo walilazimika kutoa taarifa wazirudishe kwao na watume tena kwenye akaunti sahihi ya shirikisho hali iliyochukua mda mrefu.
Akipokea fedha hizo mmoja wanariadha hao Anjelina Tsere alimshukuru Mtaka kwa kutimiza ahadi hiyo ambayo walishaikatia tamaa ya kuipata tena ambapo amesema hali hiyo imerudisha Imani yao kwa shirikisho na kuahidi kufanya vema zaidi mwaka huu.
“Kwanza nitumie nafasi hii kukushukuru Rais kwa kutimiza ahadi hii maana ilitugharimu sana nguvu zetu hivyo kimya cha mda mrefu cha viongozi wetu ilitufuta kabisa matumaini ya kupata fedha hizi lakini leo tumepata ni jambo jema na imetutia moyo katika mapambano ya kuelekea mashindano ya nyika ya dunia tunaahidi tutafanya vema zaidi”
Kwa upande wake kocha mwandamizi wa riadha nchini Zacharia Barie alisema kuwa hatua ya shirikisho kulipa madeni hayo yatarahisisha kazi za makocha watakaopata nafasi ya kuwanoa wakiwa kambini na kuwataka wanariadha kulipa fadhila hiyo waliyotendewa huku wakiiamini shirikisho lao.

No comments:

Post a Comment

Pages